Mbunge wa Ilala mheshimiwa Mussa Zungu leo amefungua mashindano ya Airtel Rising Stars mkoa wa Dar es Salaam na kuwataka vijana kucheza kwa kujituma ili kuwa wachezaji bora na hatimaye kulinusuru taifa na matokeo mabaya katika medani ya kimataifa.

Zungu amelitaka Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) kuhakikiha kwamba timu zote za ligi kuu na daraja la kwanza zinakuwa na timu za vijana. “Kwa bahati nzuri, mashindano ya Airtel Rising Stars yamewapa fursa nzuri na ni vema makocha wa ligi kuu wakayatumia kupata vijana wenye vipaji na kuwaendeleza”, alisema.

Alisema mbali ya kuwa jukwaa la kubaini wachezaji wenye vipaji, Airtel Rising Stars pia yanawahamasisha vijana kushiriki mazoezi hivyo kuwa na afya njema ili kukabiliana na masomo yao.

Aliwaambia vijana kwamba kwa dunia ya leo mpira ni chanzo cha kutumainiwa cha ajira kwa mamilioni ya vijana ambao wanaishi maisha mazuri kwa kuwa wanalipwa mishahara mizuri.

Aliwataka viongoizi wa soka kuchagua wachezaji watakaoshiriki fainali za taifa kwa kuzingatia uwezo na siyo upendeleo wa aina yoyote. Wakati mashindano ya mkoa yakiendelea makocha watateua vijana wenye vipaji kuwakilisha mikoa yao kwenye fainali ya taifa.

Kwa upande wake Rais wa TFF Jamal Malinzi ameishukuru kampuni ya Airtel kwa kubuni programu hii ili kutumika kama jukwaa linatotumika kubaini vipaji vya wanasoka chipukizi. Alisema kuwa mashindano ya Airtel Rising stars yameifanya kazi ya TFF ya kutafuta vipaji vya soka kuwa rahisi zaidi.

Akizungumza kwenye hafla hiyo, Mkurugenzi wa IT wa Airtel Tanzania Franky Filman amewashukuru wadau wote wa soka kwa kuyaunga mkono mashindano ya Airtel Rising Stars na kuyapa umuhimu yanaostahili. Pia amewataka makocha kutumia mashindano hayo kuimarisha vikosi vyao.

Mashindano ya Airtel Rising yanajumuisha mikoa ya kisoka ya Ilala, Temeke, Ilala Morogoro, Mbeya, Mwanza na Arusha itahitimishwa kwa michuano ya taifa itakayofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Karume jijini Dar es Salaam kuanzia Septemba 11 hadi 21.

Mbunge wa Ilala Musa Zungu akisalimiana na wachezaji wakati akifungua rasmi mashindano ya Airtel Rising Stars. Leo Jijini Dar-es-Salaam.
Mbunge wa Ilala Musa Zungu akiongea na wachezaji wakati wa ufunguzi wa mashindano ya Airtel Rising Stars Mbeya, Leo jijini Dar-es-Saam.
Mbunge wa Ilala Musa Zungu akipiga mpira kuashiria ufunguzi wa mashindano ya Airtel Rising Stars Mbeya, Leo jijini Dar-es-Saam.
Mkurugenzi wa IT wa Airtel Frank Filman akiongea wakati wa ufunguzi wa mashindano ya Airtel Rising Stars Mbeya, Leo jijini Dar-es-Saam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...