Mpendwa Mama Rhoda Cleopa Msuya
Daima tutakupenda kamwe hatutokusahau.
Ni Miaka kumi tangu ulipotangulia
Tumebaki na kumbukumbu za mapenzi yako ya dhati na wema wako
Tumekukumbuka leo, jana, juzi na siku kabla yake
Tunakukumbuka moyoni na kila tunapotaja jina lako
Kumbukumbu zetu kwako haziwezi kuelezeka
Tumebaki na kumbukumbu ya tabasamu lako na picha yako
Ni kumbukumbu za upendo wako ndio zinatupa nguvu ya kuendelea mbele
Daima utabaki katika mioyo yetu
Uko Katika Ufalme wa Mungu, Tunakuombea upumzike kwa amani.
Unakumbukwa daima na mume wako Cleopa, watoto wako George,John,Joyce, Job, Naanjela.
Wakwe, Onesmo, Khadija,Mercy,Mary na Yoko, wajukuu, ndugu na marafiki.
Misa maalum ya kumbukumbu ya wapendwa wetu Mama Rhoda Cleopa Msuya na Geoffrey Cleopa Msuya itafanyika Tarehe 9 August 2015 kwenye kanisa la Azania Front Cathedral saa tatu na nusu asubuhi,
Wote mnakaribishwa.
“kuwakumbuka wenye haki huwa na baraka” Mithali 10:7
Mungu azidi kukupumzisha kwa amani mama yetu! Jirani yetu!
ReplyDeletePoleni sana Job
ReplyDelete