Waziri wa Uchukuzi Samwel Sitta akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani juu ya kuchukua hatua kubwa kuanza kufufua reli ya kati muda wowote, ujenzi wa reli hiyo utaanza ili kuongeza kasi ya maendeleo hapa nchini leo Jiji Dar es Salaam.
Waandishi wa habari walio hudhulia katika mkutano na Waziri wa Uchukuzi Samwel Sitta, wakimsikiliza kwa makini.
(Picha na Emmanuel Mssaka.
Na
JenikisaNdile –Maelezo
SERIKALI kwa
kushirikiana na kampuni ya reli Asset holding imejizatiti kuimarisha miundo mbinu ya reli itakayogharimu Tsh. Trilioni 16 katika kuleta maendeleo endelevu hapa nchini.
Akizungumza na
waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam waziri wa uchukuzi Mhe. Samweli
sitta amesema kuwa mkakati ni
kuimarisha reli katika maeneo mbalimbali hapa nchini.
Aliongeza kuwa maeneo
yatakayonufaika na uboreshwaji wa miundo mbinu hiyo ni pamoja na Songa Mpiji.
Mtwara hadi Mbambabay, Songea hadi Mchuchuma na mradi mpya wa reli ya kutoka
Dar es Salaam hadi Bagamoyo.
“Lengo la miradi hii ni kuhakikisha kuwa tunaleta
maendeleo ya kiuchumi kwa kujipatia
fedha za kigeni ambazo zitatokana na
usafirishaji wa mizigo nje ya nchi “ amesema Mhe. Sitta.
Aliongeza kuwa miradi
hiyo inatarajiwa kuanza mwanzoni mwa mwezi wa tisa ambapo Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa
Tanzania Mhe. Dkt.Jakaya Kikwete ataweka jiwe la msingi tayari kwa utekelezaji.
Aidha alibainisha kuwa
kwa kuimarisha miundo mbinu ya reli kutasaidia katika kurahisisha usafirishaji
wa mizigo yenye uzito mkubwa kama mafuta, makaa ya mawe na chuma ndani na nje
ya nchi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...