KUSOMA  ZAIDI  kliks  goes  to  sheriayakub.blogspot.com
Na  Bashir  Yakub.

MARA  kadhaa  mkopaji  anaposhindwa  kulipa  mkopo  hukimbilia  mahakamani  ili  kuona  kama  anaweza  kupata unafuu  hasa linapokuja  suala  la  wakopeshaji  wake  kutaka  kuuza    nyumba/kiwanja  alichoweka  rehani.  Ni  ukweli  usiopingika  kuwa  hatua  hii  imewasaidia  wengi  hasa  wale  wanaowahi.  Yapo  makala   tuliwahi  kuandika kuhusu  hatua  za kuchukua  hasa  inapotokea  kuwa  nyumba  yako  inataka  kuuzwa.

 Makala  yalieleza  namna na hatua  za  kufuata ili  kuokoa  nyumba.  Kwenda  mahakamani  kuzuia  nyumba  isiuzwe  baada  ya  kushindwa  kurejesha  kiasi  cha  rejesho  sio ukorofi  isipokuwa ni  kutekeleza  lililo  ndani  ya  sheria hasa  pale panapo  sababu  za  msingi  za  kufanya  hivyo.

 Mahakama  za  ardhi  za  wilaya  na  mahakama  kuu  hasa  ya  ardhi  ndizo  mahakama  zenye  mamlaka  katika  kutoa  mazuio  haya  kutegemeana   na thamani  ya  nyumba/kiwanja  na kiasi  cha  deni  kilichohusishwa  katika  muamala  huo. 

Swali  kwetu ni  kama  baada  ya  kuwa  umeenda  mahakamani  na  kubahatika  kupata  zuio la kutouzwa  nyumba  yako, je  upande  wa  wakopeshaji  wanaweza kukata  rufaa  kupinga  amri  hiyo na  kufanikiwa. Majibu  ya  swali  hili ndio  makala  ya  leo.

1.HAKI  YA  RUFAA.
Kifungu  cha  74   cha  sura  ya  33 Sheria  mwenendo  wa  madai kinaeleza  rufaa  katika  amri  mbalimbali  za  mahakama.  Kifungu  kilieleza  wazi  kuwa  kutakuwa  na  rufaa  kutoka  mahakama  za  wilaya  na  zile  za  hakimu  mkazi  ambapo  rufaa  hizo  zitatakiwa  kwenda  mahakama  kuu. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...