KUSOMA ZAIDI kliks
goes to sheriayakub.blogspot.com
Na Bashir
Yakub.
MARA kadhaa mkopaji
anaposhindwa kulipa mkopo
hukimbilia mahakamani ili
kuona kama anaweza
kupata unafuu hasa linapokuja suala
la wakopeshaji wake
kutaka kuuza nyumba/kiwanja alichoweka
rehani. Ni ukweli
usiopingika kuwa hatua
hii imewasaidia wengi
hasa wale wanaowahi.
Yapo makala tuliwahi
kuandika kuhusu hatua za kuchukua
hasa inapotokea kuwa
nyumba yako inataka
kuuzwa.
Makala yalieleza
namna na hatua za kufuata ili
kuokoa nyumba. Kwenda
mahakamani kuzuia nyumba
isiuzwe baada ya
kushindwa kurejesha kiasi
cha rejesho sio ukorofi
isipokuwa ni kutekeleza lililo
ndani ya sheria hasa pale panapo sababu
za msingi za
kufanya hivyo.
Mahakama
za ardhi za
wilaya na mahakama
kuu hasa ya
ardhi ndizo mahakama
zenye mamlaka katika
kutoa mazuio haya
kutegemeana na thamani ya
nyumba/kiwanja na kiasi cha
deni kilichohusishwa katika
muamala huo.
Swali kwetu ni
kama baada ya
kuwa umeenda mahakamani
na kubahatika kupata
zuio la kutouzwa nyumba yako, je
upande wa wakopeshaji
wanaweza kukata rufaa kupinga
amri hiyo na kufanikiwa. Majibu ya
swali hili ndio makala
ya leo.
1.HAKI YA
RUFAA.
Kifungu cha 74 cha
sura ya 33 Sheria
mwenendo wa madai kinaeleza rufaa
katika amri mbalimbali
za mahakama. Kifungu
kilieleza wazi kuwa
kutakuwa na rufaa
kutoka mahakama za
wilaya na zile
za hakimu mkazi
ambapo rufaa hizo
zitatakiwa kwenda mahakama
kuu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...