SHIRIKA la Majisafi na Majitaka Dar es salaam (DAWASCO) limezindua rasmi kampeni yake mpya inayojulikana kama “MAMA TUA NDOO KICHWANI” kampeni ambayo ni endelevu inayolenga kuboresha huduma ya Maji safi na salama maeneo yote  ya jiji la Dar es salaam, pamoja na miji yote ya Kibaha na Bagamoyo mkoani Pwani, huku ikimhakikishia mwanamke kumpunguzia adha ya kutafuta Maji kutoka umbali mrefu.

Akizungumza kwenye uzinduzi wa kampeni hiyo, Afisa mtendaji mkuu wa Dawasco, Mhandisi Cyprian Luhemeja amesema kuwa kampeni hiyo ina malengo ya kusogeza huduma ya Maji karibu kwa kuhakikisha inaongeza wigo wa huduma ya Maji safi na salama kwa kujenga vituo takribani 18 ambavyo vitakuwa vikitoa huduma ya Maji kwa wateja wake kwa muda wa saa 24 kupitia wakala wake.

Katika uzinduzi wa kampeni hiyo, Mhandisi huyo pia alitoa rasmi kibali cha kuuza Maji kwa watu wote wenye visima na magari makubwa (Maboza) huku akifanya usajili bure kwa wauzaji hao wa Maji na wamiliki wa visima waliohudhuria uzinduzi wa kampeni hizo, aliwataka wenye matanki kuacha kuchota Maji sehemu ambazo sio rasmi kwani kwa kufanya hivyo wanahatarisha afya ya watumiaji wa huduma hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...