Rais Joseph Kabila wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) akiwa amebeba kombe la ubingwa wa CHAN2016 katika picha ya pamoja na wachezaji na viongozi wa timu ya Taifa ya nchi hiyo 'Leopards' Ikulu ya Kinshasa mwishoni mwa juma ambapo alimzawadia kila mchezaji gari aina ya Prado. Pamoja na magari Rais Kabila pia alimpa kila mchezaji Medali maalum ya Kutukuka katika michezo (Sporting Merit). Yote hii ni baada ya kuichapa Mali bao 3-0 Jumapili katika mchezo wa fainali ya michuano hiyo ambayo ni kwa wachezaji wa ligi za ndani barani Afrika. Mwaka 2009 DRC walichukua kombe hilo pia wakati wa kuanza kwa michuano hiyo.

 Sehemu ya magari waliyozawadiwa wachezaji wa Timu ya Taifa ta DRC 'Leopards' baada ya kunyakua kombe la CHAN2016

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...