Hali ya simanzi yaukumba mkoa wa Geita baada ya radi kuua watu 3 wa familia moja kufuatia mvua kubwa zinazoendelea kunyesha.https://youtu.be/xCc2OKhSG9k  

Uongozi wa Mgodi wa Tanzanite One ulioko Mererani wawafukuza wafanyakazi 201 kwa tuhuma za kufanya mgomo usio halali na kuharibu miundombinu. https://youtu.be/cxX13rhIA1Y   

Zaidi ya mifugo 200 wilayani Mvomero mkoani Morogoro wakatwakatwa mapanga na wakulima wakiwatuhumu wafugaji kulisha mifugo yao katika mashamba yao. https://youtu.be/pCEZ-MAnjLQ  

Shule ya msingi Majengo iliyoko manispaa ya Songea mkoani Ruvuma yaelezwa kutokuwa na huduma ya choo tangu kuanzishwa kwake. https://youtu.be/xAmiu2PbrpY  

Idara ya mahakama nchini yajipanga kuanza ujenzi wa mahakama katika ngazi 4 ikiwemo mahakama za mwanzo, wilaya, mkazi na mahakama kuu baada ya kupokea shilingi bilioni 12 kutoka serikalini. https://youtu.be/at6dBSY84Y8  


Serikali yasema ipo katika mchakato wa kuboresha shirika la ndege Tanzania ATC ili liweze kufanya kazi kibiashara;https://youtu.be/OqeXaIR5M7Q

Serikali yasema itaunda upya kikosi cha kulinda wanyapori ili kupambana vilivyo na suala la ujangili nchini;https://youtu.be/_LqK_RQ279k  

Serikali yasema inaanza kuangalia ujuzi unaotolewa kwa wanafunzi wa vyuo vikuu nchini kama unachangia maendeleo ya wananchi pamoja na kukuza uelewa miongoni mwa  wanafunzi husika;https://youtu.be/sNtvDrVhv6s  

Wazee katika kambi ya Kalwande mkoani Mwanza  waiomba serikali iwasaidie msaada wa chakula; https://youtu.be/Hgaq7-ML944   

Jeshi la polisi visiwani Zanzibar lapiga marufuku vitendo vya kusamba vipeperushi vyenye ujumbe wa vitisho;https://youtu.be/QbddFe9Qo10  

Mradi wa ujenzi wa barabara kwa ajili ya kupunguza foleni katika jiji la Dar es Salaam kukamilika mwezi Juni mwaka huu;https://youtu.be/d9tmm8pPLGw  

Mkuu wa chuo kikuu cha Dar es Salaam, Dkt Jakaya Kikwete aahidi kuendeleza upanuzi na uboreshaji wa chuo hicho;https://youtu.be/M9rnBG3TnkU  

Wabunge wa mkoa wa Kigoma wameunda umoja wa kushughulikia mipango ya maendeleo kwa ajili ya mkoa huo;https://youtu.be/fG2D3ldrvPw  

Serikali imebuni na kutekeleza sera ya kumuwezesha mwananchi kiuchumi ili mwananchi aweze kufaidika na rasimali zilipo nchini;https://youtu.be/XeSmBQEUwFw  

Serikali yawataka wafanyabiashara nchini kulipa kodi zao kikamilifu ili kuiwezesha serikali kutimiza ahadi yake ya kuwahudumia wananchi; https://youtu.be/-Pknr0z76M8  

Timu ya Yanga inatarajiwa kuondoka kesho kuelekea Mauritius kwa ajili ya mchezo wake wa ligi ya mabingwa dhidi ya timu ya Cercle de Joachim; https://youtu.be/_YzshddYyDc  

Inaelezwa watu wasiojulikana  katika mkoa wa kusini  visiwani Zanzibar wazichora alama ya  X nyumba zipatazo 31 zinazosadikiwa kuwa ni za wanachama wa Chama Cha Mapinduzi CCM;https://youtu.be/9A8H2xKiDZg  

Serikali wilayani Magharibi visiwani Zanzibar yasitisha ujenzi wa kituo cha kuhifadhi mafuta  katika eneo la Mtoni;https://youtu.be/3MQvVHF3oaA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...