Baadhi ya abiria waliokuwa wamepanda kivuko cha Mv Kigamboni wakiwa wamekumbwa na butwaa kufuatia kivuko hicho walichokuwa wamepanda kukatika sehemu ya kushukia abiria na Magari na kupelekea hofu kubwa miongoni mwao,kama uonavyo pichani baadhi ya abiria hao wakijaribu kujinusuru na hali hiyo,kwani kivuko hicho kilikuwa kimesheheni abiria lukuki
Abiria wakipewa maelekezo namna ya kushuka kwenye kivuko hicho.
Tafadhalini wahusika ni lazima kifanyike kitu cha haja na haraka ili kunusuru umati wa binadamu uishio Kigamboni. Kama kweli maoni haya yanafika tunamuomba Rais Magufuli na watendaji wengine tulione hili na kuepusha kukosa roho za wapendwa wetu.Kuna kila dalili kuwa pale ni lazima kifanyike kitu kuweza kuzuia mabalaa haya. leo tumeshhudia kuwa wale wote wanaovaa magwanda ya kibuluu na kutuswaga plae Ferry milangoni hawana elimu wala uelewawowote wa nini kifanywe wakati wa taharuki kama ile. Mungu ibariki nchi yetu hii.
ReplyDelete