Na  Bashir  Yakub.

Marehemu  atakapokuwa   ameacha  shauri  mahakamani  ambalo  alikuwa  anashtakiwa nalo  kabla  ya  kufa  kwake  basi  hukumu  itakapotoka  itatakiwa  kutekelezwa.  Hapa  tunaongelea  hukumu  itokanayo na mashauri  ya  madai. Sambamba na  hilo makala  yataangalia  pia mambo  kadhaa  yanayohusu  kifo  cha  mtu  ambaye  alikuwa  akishitakiwa/akilalamikiwa  mahakamani kabla  ya  kifo  chake. Amri  ya  xxii  kanuni  ya  1 – 12  ya  sheria  ya  mwenendo  wa  mashauri ya madai  ndiyo  itakayotuongoza.

1.JE MSHITAKIWA  AKIFA  NA  KESI  ITAKUFA.

Kanuni  za  jumla (general rule)   ni  kwamba  shauri  hutakiwa  kufunguliwa  na  mtu  aliye  hai  dhidi/akimshitaki  mtu  aliyehai. Hii  ni  kanuni  ya  jumla  yenye  kumaanisha kuwa  mtu  aliyekufa  hawezi  kushtaki  wala  kushtakiwa. Hata  hivyo  kwenye  kanuni  za  sheria  pale  penye  kanuni  ya  jumla( general rule)  huwa  kuna  vinginevyo( exception).  Hii  ina  maana  yapo  mazingira  ambapo  mshitakiwa  atakufa  lakini  kesi  yake  haitakufa  itaendelea. 

2. KESI KUENDELEA HATA  BAADA  YA  KIFO  CHA  MSHITAKIWA/MLALAMIKIWA.

Ikiwa  marehemu  alikuwa  ameshtakiwa/amelalamikiwa   katika  kesi  ambazo  zinahusu  mali  kama  nyumba, gari, kiwanja  na  mali  nyinginezo   na  akafa kabla  ya  kesi  hiyo  kuisha  basi  kesi  hiyo  itaendela.  Pia  ikiwa  alishitakiwa  katika  mashtaka yanayohusu   masuala  ya  mikataba  pia  kesi  hiyo nayo  itaendelea.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...