Baadhi ya waandishi wa kigoma wakimsikiliza ofisa wa TMF Dustan Kamanzi(hayupo pichani) wakati akilezea Tanzania Media Foundation mpya na jinsi ya kuomba ruzuku
Ofisa Wa TMF  wa ruzuku  za vijijini  Dustan Kamanzi akiwaelezea waandishi wa Kigoma juu ya TMF mpya na jinsi ya kuomba ruzuku za vijijini kwa mwandishi mmoja mmoja.
Ofisa wa TMF Razia Mawanga akiwaeleza waandishi wa Kigoma juu ya TMF mpya na jinsi ya kuomba ruzuku za mashirika

Editha Karlo, wa blog ya jamii, Kigoma

TANZANIA Media Fund(TMF) wameitambulisha TMF mpya kwa waandishi wa habari wa Mkoa wa Kigoma na kuwataka waandishi kuomba ruzuku zinazotolewa sasa kwa mfumo mpya. Akiilezea TMF mpya ofisa wa ruzuku za vijijini TMF Dustan Kamanzi alisema kuwa sasa hivi utaratibu umebadilika na umeboreshwa kwa waandishi na mashirika watakayoomba ruzuku. 

Alisema waandishi watakaoenda kufanya kazi za vijijini watapewa ruzuku ya shilingi milioni 4 ambayo wataifanyia kazi kwa kipindi cha miezi mitatu kwa kuandika makala nne au vipindi vya radio na television.

Kamanzi alisema kuwa kwa upande waandishi mmoja mmoja watakaomba ruzuku lazima ya vijijini au mjini na habari hizo lazima zilenge watu waliosahaulika au kutengwa na jamii. Alisema ruzuku hizo zinalenga kuongeza ubora wingi na anuwai za sauti na masuala ya watu wa kawaida katika vyombo vya habari. 

Alisema ruzuku hizo zitawapa kipaumbele waandishi wanawake, waandishi chipukizi, waandishi wa kati na wenye hari ya kuandika habari za vijijini pia wenye uhakika wa wa kupata vyombo vya kutolea habari zao. 

Naye Razia Mawanga alizungumzia ruzuku za taasisi kuwa zinalengo la kuviwezesha vyombo vya habari na taasisi za habari kutengeneza maudhui maalum yatakayovutia jamii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...