Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

BARAZA la wazee wa Yanga wameomba kupewa ufafanuzi na Shirikisho la Mpira wa Miguu (TFF) pamoja na Baraza la Michezo nchini (BMT) kuhusiana na matumizi ya kadi zitakazoruhusiwa kupiga kura siku ya uchaguzi, kwani hilo limekuja baada ya taarifa kutolewa kuwa kadi za zamani ndizo zitakazotumika katika siku ya kupiga kura.

Katibu mkuu wa baraza hilo, Ibrahim Akilimali amesema wanataka ufafanuzi zaidi kwani toka kuanza kwa mfumo wa kadi mpya za benki ya Posta wanachama wengi walibadilisha na kuondoka kwenye mfumo huo zamani na kadi hizo wanazitumia kwa miaka miwili sasa.

"Kutokana na tamko lao la kutumia kadi za zamani na kuwabagua wale wenye kadi mpya na kusema walio na kadi za zamani ndiyo wanahaki ya kupiga kura kiuhalisia inaweza kuleta mgogoro kwa wanachama,"amesema Akilimali. Kwahiyo tunaomba TFF na BMT kuweza kutoa tamko la kutumika kwa kadi zote mbili kwani hata katika uchaguzi wa mwaka 2006 zilitumika kadi mbili Yanga kampuni na Yanga Asili.

Pia, Baraza la wazee limeombaTFF na BMT kuipa ruhusa Sekretarieti ya Yanga kuitisha mkutano mkuu wa dharura wa wanachama wenge Ajenda ya uchaguzi mkuu ili wanachama wapewe taarifa kuhusu uchaguzi, na katika mkutano huo sekretarieti iwaalike viongozi kutoka wizara husika, TFF, DRFA (chamacha mpira wa miguu mkoa wa Dar es salaam) na wadau wote ili kushuhudia maamuzi ya wanachama wa Yanga huku wakiomba busara itumike na kudumisha umoja, amani na utulivu uliopo ndani ya klabu hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...