Na  Bashir  Yakub.

1.WAKFU  NININI.
Sheria ya  Mirathi na  Usimamizi  Mali Sura  ya  352  ndiyo  sheria  inayoeleza  masuala  yote  ya  msingi  kuhusu   habari  nzima  ya  Wakfu.  
Kwa  mujibu  wa  sheria  hiyo kifungu  cha  140  Wakfu  ni  kutoa  mali  kulingana  na    sheria  za  kiislam  kwa  ajili  ya  dini, hisani  au  kwa  ajili  ya watu/mtu  wa  familia  fulani. 
Suala  la  Wakfu  huenda  sambamba   na  suala  la  wadhamini.  
Kwa  mujibu  wa  kifungu  hicho  wadhamini  ni  watu/mtu  ambaye  
ndiye   hupewa  jukumu  la  kusimamia  mali  ya  wakfu.  
Kama  ni  nyumba  yenye  wapangaji  basi mtu  au  watu  hao  ambao  ni  wadhamini  ndio  watahusika  
na  kukusanya  kodi  pamoja  na  mambo  mengine  yote  yanayohusu   
nyumba. Na  kama  kuna  maendelezo  yoyote ya ukarabati  au  vinginevyo   hawa  ndio  watahusika.

2.  MAELEKEZO YA  MTOA  WAKFU LAZIMA YAFUATWE.
Siku  zote  mtoa  wakfu  hutoa  mali  kwa  malengo  maalum. Yaweza  kuwa  malengo  ya  kiimani  au  vinginevyo. Mtoa  wakfu  anapotoa  nyumba/kiwanja  kama  wakfu  
hutoa  kwa  maelekezo  ya  namna  na  jinsi  kitakavyotumika. Kwa  namna  mtoa  wakfu  atakavyotoa  maelekezo  ndivyo  hivyo  
inavyotakiwa  kuwa. 
Ni  kosa  mali  ya  wakfu  kutumika   kinyume  na  maagizo  ya  mtoa  wakfu. Ikiwa  itatumika  kinyume  basi  kuwe  na  sababu  za  msingi  
ambazo  zinalazimisha  hivyo. Ziwe  ni sababu  ambazo hakuna  namna  isipokuwa  ni  lazima kufanyika  hivyo.  Kifungu  cha  150
(  1  ) cha  sheria  ya  mirathi  na  usimamizi  wa  mali  kinasema  kuwa  matumizi  ya mali  za  wakfu  ni  lazima  yazingatie  nia  na  malengo  ya  mtoa  wakfu. 

Isipokuwa  kifungu  hicho  kinasisitiza  kuwa  nia  na  malengo  ya  mtoa  wakfu  yatafuatwa  tu  pale  ambapo   nia  na  malengo  hayo  yatakuwa  halali  kisheria. Ikiwa  mtoa  wakfu  ameelekeza  matumizi  ambayo   hayakubaliki  kisheria  basi  maelekezo   hayo hayatafuatwa.  Lakini ikiwa  hayapingani   na  sheria  yoyote  basi  ni  sharti  kuyafuata.
KUSOMA  ZAIDI sheriayakub.blogspot.com

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...