Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli atakuwa
mgeni rasmi katika ufunguzi wa Mkutano wa mashauriano wa Bodi ya Usajili wa
Makandarasi Nchini (CRB) kesho Alhamisi tarehe 26 Mei, 2016 katika ukumbi wa Diamond
Jubilee jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa Eng. Joseph M. Nyamhanga, Katibu Mkuu (Ujenzi),Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na
Mawasiliano, mkutano
huo wa mwaka wa mashauriano na wadau wa Bodi ya Usajili wa Makandarasi
unatarajiwa kuhudhuriwa na zaidi ya Makandarasi
na wadau wa Sekta ya Ujenzi wapatao 1000 na utafanyika kwa siku mbili kuanzia
tarehe 26 Mei, 2016 hadi tarehe 27 Mei 20l6.
Kaulimbiu
ya mwaka huu ni ‘Juhudi za Makusudi za
Kukuza Uwezo wa Makandarasi Wazalendo kwa Maendeleo Endelevu ya Kiuchumi; Changamoto
na Mustakabali Wake’.
Katibu Mkuu huyo amebainishwa kuwa Lengo
la mkutano huu ni kuwakutanisha wadau wa Bodi ya Usajili Makandarasi na Sekta
ya Ujenzi ili kujadili changamoto zinazowakabili na kuweka mikakati ya kuwajengea
uwezo Makandarasi Wazalendo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...