Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni(Mb) akitoka katika lango Kuu la Gereza Msalato alipofanya ziara ya kikazi katika Gereza hilo leo Mei 29, 2016 Mkoani Dodoma(kushoto) ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, CGP John Casmir Minja.
Kamishna Jenerali wa Magereza, CGP John Casmir Minja(wa pili kulia) akiwa ameongozana na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni(wa kwanza kushoto) na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira(wa pili kushoto) walipofanya ziara ya kikazi katika Gereza Msalato lililopo Mkoani Dodoma(wa kwanza kulia) ni Mkuu wa Magereza Mkoa wa Dodoma, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Antonino Kilumbi.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni(kushoto) akiongea na Wafungwa wa Gereza Msalato(hawapo pichani) alipofanya ziara ya kikazi gerezani hapo(katikati) ni Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira(kulia) ni Kamishna Jenerali wa Magereza, CGP John Casmir Minja kwa pamoja wakisikiliza kero mbalimbali za Wafungwa
Muonekano wa eneo la Gereza Msalato ambalo linajishughulisha na mradi wa upondaji wa kokoto kama inavyoonekana katika picha.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza nchini, CGP John Casmir Minja akifanya mahojiano maalum na Waandishi wa Habari mara baada ya kutembelea eneo la mradi wa kuponda kokoto katika Gereza Msalato lililopo Mkoani Dodoma(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akipokea saluti kutoka kwa Mkuu wa Gereza Msalato, Mrakibu Mwandamizi wa Magereza, Stevin Mwihambi alipowasili Gerezani hapo kwa ziara ya kikazi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...