Na: Lilian Lundo – MAELEZO

 Waimbaji wa Nyimbo za Injili nchini wametakiwa kuifanya kazi hiyo kwa kujitolea ikiwa kama sehemu ya ibada ya kumtumikia Mungu kwa kulitangaza neno lake na si kugeuza kazi hiyo kuwa mtaji wa biashara.

Hayo yamesemwa na Mwalimu wa kwaya ya Wateule Elikana Simatiya kutoka kanisa la Anglikani, St. James lililoko Tabata Segera jiijini Dar es Salaam, maarufu kama  kunyata nyata  jina lililotokana na nyimbo ya kunyata nyata aliyoifundisha akiwa kwaya ya Mennonite. 

“Waimbaji wengi wa nyimbo za injili wameacha kutumikia Mungu na badala yake   wamekuwa wakiuunda vikundi binafsi vya uimbaji ambavyo hutumika kama vyanzo vya fedha na hualikwa kwenye mikutano ya injili na sherehe mbalimbali kwa malipo maalum,” alisema Simatiya.

Aidha ameeleza kuwa, uimbaji wa nyimbo za injili ni wito kama ulivyo wito wa uchungaji lakini hivi sasa muimbaji wa injili akialikwa katika mikutano ya injili au sherehe huomba malipo hadi ya shilingi milioni moja.

Simatiya aliongeza kuwa, ziko gharama ambazo muimbaji anaweza kuomba kupewa kama usafiri kwa ajili ya kumfikisha eneo husika au malazi na chakula ikiwa atahitajika kulala nje ya makazi yake, lakini waimbaji wa leo wamebadilisha wito wa kutangaza injili kwa njia ya uimbaji kuwa biashara.
Hivyo mwalimu huyo amewataka waimbaji kubadilika kwa kuacha kuharibu kazi ya Mungu na kufanya kazi hiyo kwa kujitolea kwani wapo wanaopokea uponyaji na wanaotiwa moyo kupitia nyimbo za injili.

Kwaya ya Wateule inatarajia kuzindua albamu mpya ijulikanayo kama Wateule tutakwenda siku ya Jumapili Mei 29, 2016 Tabata Segerea katika kanisa la St. James, ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda,huku wakisindikizwa na  waimbaji wa injili ambao ni Ambwene Mwasongwe, Christina Shusho, Edson Mwasabwite pamoja na kwaya za Anglikan kutoka Vingunguti na Ukonga.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...