Waziri wa Mambo ya nje Ushirikano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga (aliye shikilia funguo za gari), akipokea Ufunguo wa Magari ya Wagonjwa kutoka kwa Balozi wa Korea Kusini nchini, Mhe. Song Geum Young yaliyotolewa Serikali ya nchi yake. Waziri Mahiga alitumia nafasi hiyo Kuishukuru na kuipongeza Serikali ya Korea Kusini kwa msaada huo ambo utatumika kwenye Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na Hospitali ya Rufaa ya Bugando Mwanza. Tanzania na Korea Kusini zina mahusiano mazuri, ambapo Korea Kusini inaendelea kuisaidia Tanzania kwenye sekta mbalimbali zikiwemo afya,miundombinu, elimu na uchumi. 
Waziri Mahiga akijaribisha moja ya magari aliyokabidhiwa na Serikali ya Korea Kusini kupitia Balozi Young kushoto. 
Picha ya Magari yaliyotolewa kwa msaada wa Serikali ya Korea Kusini.
Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mbelwa Kairuki (wa kwanza kushoto), Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Mindi Kasiga (wa kwanza kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Korea Kusini Mhe. Song Geum Young mara baada makabidhiano ya magari kwa Mhe. Dkt. Mahiga (hayupo pichani).Picha na Reginald Philip

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...