Mkurugenzi wa Ubunifu wa Shirika la Nyumkba la Taifa la Tanzania (NHC), Issack Peter akitoa mada kuhusu utendaji wa Shirika hilo jijini Dar es Salaam wakati wa mkutano wa kujifunza utekelezaji mradi wa ECO Residence uliojengwa na NHC Kinondoni Hananasifu na kujadili mapendekezo ya mradi huo.
PICHA ZOTE NA PHILEMON SOLOMON-FULLSHANGWEBLOG.
Prof Ninatubu Lema ,kutoka Chuo cha Uhandisi na Teknolojia (CoET) akisisitiza jambo wakati wa mkutano wa kujifunza utekelezaji wa mradi ECO Residence na kujadili mapendekezo ya mradi huo.
Wadau mbalimbali wa sekta ya ujenzi wakifuatilia mada mbalimbali wakati wa mkutano wa kujifunza utekelezaji mradi wa ECO Residence na kujadili mapendekezo ya mradi huo.
Wafanyakazi wa Shirika la Nyumkba la Taifa la Tanzania (NHC) wakimsikiliza Mkurugenzi wa Ubunifu wa Shirika hilo, Issack Peter wakati akitoa ufafanuzi kuhusiana na malengo ya uendelezaji wa mradi huo.
Ni muonekano mzuri wa kisasa tuendelee kuchangia ujenzi wa nyumba bora hasa za gharama nafuu, ziwe na bei ambayo watanzania wanaweza kuimudu.
ReplyDeleteTujifunze kutoka nchi ya jirani ina over supply ya office space na nyumba za kuishi sehemu nyingine, siyo kwa sababu wameweza kukidhi mahitaji ya nyumba ila ni kwa sababu wengi hali yao ya kipato haiwezi kumudu makazi ya gharama ya juu. Matokeo yake bei ya pango hali ikiendelea ya kukosa wapangaji wenye uwezo wa kulipa itabidi ishuke au nyumba ziuzwe ili mikopo ilipwe.