Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini inapenda kuwafahamisha wananchi kwamba, kuanzia tarehe 27 Juni, 2016 hadi tarehe 06 Julai, 2016 itaendesha zoezi la uhakiki wa utekelezaji wa masharti ya usajili na matakwa mengine ya Sheria ya Vyama vya Siasa ya Mwaka 1992, kwa Vyama vya Siasa vyenye usajilli wa kudumu kwa upande wa Tanzania Bara.
Zoezi hili ni endelevu kwani ni utekelezaji wa kawaida wa majukumu ya Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa.Hufanyika kila mwaka isipokuwa kwa mwaka jana (2015) kwa kuwa ulikuwa mwaka wa uchaguzi.
Zoezi la uhakiki kwa upande wa Zanzibar litafanyika baada ya zoezi kukamilika Tanzania Bara kwa tarehe ambazo zitatangazwa baadaye.
Ofisi inatoa rai kwa vyama vyote vyenye usajili wa kudumu kulipa kipaumbele zoezi hili, kwani ni zoezi ambalo linagusa uhai wa kila chama.
Jaji Francis S.K. Mutungi
MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA
24 JUNI, 2016
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...