Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Salum Hamduni akizungumza na waandishi habari juu ya utapeli unaofanywa na watu kwa kutumia majina ya viongozi akiwemo, Waziri Mkuu pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam.
Waandishi wa habari wakimsikiliza Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Salum Hamduni hayupo pichani leo jijini Dar es Salaam,.
(Picha na Emmanuel Msaaka,Globu ya Jamii).
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.
JESHI la Polisi Mkoa Ilala linamshikilia mkazi wa Pugu, Imarock Paula Rutashabya ‘ Issa Mohamed Jiunga’ kwa tuhuma za kutumia jina la mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kwa ajili ya kujipatia kipato kwa kupiga simu kwa watu wenye nafasi zao kwa kuomba fedha.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Salum Hamduni amesema tukio hilo lilitokea Juni 16 mwaka huu maeneo ya mtaa wa Samora Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam.
Kamanda, Hamduni amesema mtu alikamatwa baada ya kumpigia simu Mkurugenzi wa Kampuni ya Jones Logistics LTD , James Rodrick Luponda na kujitambulisha kwa jina la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam lengo la kumsaidia kijana wake aliyepata ufadhili wa kusoma lakini anahitaji achangie asilimia 30 sawa na dola za Kimarekani 35,000 ya gharama za chuo kilichoko nchini Ufilipino baada ya kupata ufadhili wa asilimia 70.
Amesema mtuhumiwa katika maongezi yake alimueleza mkurugenzi huyo kuwa fedha hizo atumie benki ya Eco akaunti Kenya au kutoa pesa taslim kwa kumpa namba za simu 0717 338 473 ya kijana anayehitaji msaada kuwa atafika ofisini kwake baada masaa mawili akiwa na nyara zote za fursa ya hayo masomo pamoja na akaunti namba ya benki alizozitaja.
Mtuhumiwa alikamatwa na anahojiwa ili kuweza kupata mtandao wake ambao wanatumia majina ya viongozi kujipatia kipato.
Majina ya viongozi ambayo yanatumika kwa watu kujipatia kipato kwa njia ya utapeli ni Waziri Mkuu , Mkuu wa Mkoa na wengine na kuahidi wananchi kutoa ushirikiano dhidi ya watu wanaotumia majina hayo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...