KAMPUNI ya Nexgen inayojishughulisha na utetezi wa Haki za watoto hapa nchini wamewapokea wanafunzi 21 wa shule ya All Saints Anglican ya nchini ya Australia.

Akizungumza na waandishi wa habari, Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Nexgen, Jacob Kahemele mara baada ya kuwapokea wanafunzi 21, wazazi wawili na walimu wawili wa shule ya All Saints Anglican ya nchini ya Australia amesema kuwa wamekuja kwaajili ya kutoa mafunzo mbalimbali kwaajili ya kumkinga mtoto wa kike ili aweze kuwa salama na kubaki salama.

Amesema kuwa nchi ya Australia ndio nchini inayoongoza katika kumlinda mtoto na kuepukana na matatizo mbalimbali yanayomkumba mtoto wa kike hasa matatizo ya kubakwa kutokana na kesi nyingi kujitokeza hapa nchini Pia amewaasa viongozi wa nchi waongeze nguvu juu ya kumlinda mtoto.

Kahemele amesema kuwa viongozi wa siasa waachane kuzungumza vitu visivyo vya msingi bungeni na adala yake waanze kufikilia juu ya kumlinda mtoto hasa wa kike ili kuepukana na matatizo mbalimbali yanayomkumba.

Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Nexgen, Jacob Kahemele akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya wanafunzi wa shule ya All Saints Anglican kuwasili katika uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam. Amesema kuwa wanafunzi hao wamekuja hapa nchini kwaajili ya kusaidi na kuhamasisha jamii kuzuia na kupambana juu ya usala wa mtoto katika maisha yake ya utoto.
 Mwalimu wa shule ya All Saints Anglican ya nchini Australia, Blendan Collaghan akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam mala baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam jana.
Wanafunzi wa Shule ya msingi ya Fountain Gate Academy wakiwapokewa na kuwafunga skafu za bendera ya Taifa wanafunzi wa shule ya All Saints Anglican ya nchini ya Australia walipowasili katika uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Nexgen, Jacob Kahemele akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa shule ya All Saints Anglican ya nchini Australia na Mwanafunzi wa shule ya msingi ya Internation ya Fontain gate Academy katika uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...