Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii.
JESHI la Polisi Mkoa wa Temeke linawashikilia waendesha bodaboda 35 kwa makosa mbalimbali ikiwemo kutovaa kofia ngumu (Helmet).

Akizungumza na  Repota wa Globu ya Jamii, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke,  Kamishina Msaidizi wa Jeshi la Polisi  (ACP), Gilles Muroto amesema kuwa kukamatwa kwa bodaboda hao kumetokana na opresheni wanayoifanya ya usalama barabarani ambayo ni endelevu.

Amesema  kuwa  wanawasiliana na mamlaka ya Usafiri wa Majini na Nchi Kavu (Sumatra) juu ya kuweza kuwafikisha mahakamani waendesha bodaboda kwa makosa ambayo wanahusika nayo.
‘’Temeke tumejipanga kuhakikisha kila mtu anayetumia chombo cha moto anafuata sheria na kanuni  na wataokwenda tofauti watafikishwa katika vyombo vya sheria’’Amesema Muroto.

Aidha amesema kuwa opresheni hiyo ni endelevu haishi leo hivyo wale ambao wanajua zimamoto wakikamatwa na makosa ambayo wanapigiwa kelele ikiwa ni usalama wao.

Muroto amesema ametaka wananchi kutoa ushirikiano wa vitendo vya kialifu ili kuweza  jeshi kufanya kazi yake na kuweza kuwakamata wale ambao wanajihusisha na uhalifu mbalimbali ndani ya Temeke.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...