Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema kuwa hali ambayo ilikuwa imefikia katika wodi za wazazi ni mbaya, kwa kulala chini ya sakafu baada ya kujifungua  au kulala wazazi wane katika kitanda kimoja.

Makonda amesema kuwa hata Rais Dk.John Pombe Magufuli kitendo hicho hafurahishwi hivyo jitihada lazima zichukuliwa kwa wazazi kuwa kitanda mmoja kwa mzazi mmoja katika hospitali ya Amana,Mwananyamala na Temeke.

Akizungumza leo wandishi wa habari wakati wakati akipokea mchoro wa ghorofa tatu zitazojengwa kila Hospitali za Rufaa katika jiji la Dar es Salaam kwa kubeba wazazi 150 kwa kitanda kimoja mazazi mmoja zitajengwa na muungano wa makampuni ya amsons, Makonda amesema  watashirikiana  na wadau ili kuhakikisha wanamaliza tatizo la mazingira mabaya katika utoaji wa huduma za afya.

Amesema ufadhili wa ujenzi wa majengo hayo umetolewa na Kampuni ya Amsons ambao watajenga majengo yote kwa gharama zao.
Amsema ujenzi huo  kina mama na watoto wamekuwa wakitseka wanalala kitanda kimoja wawili hadi wanne naona mwisho umefika naomba wadau kuendelea kujitokeza kusaidia sekta mbalimbali hasa  huduma za afya," alisema Makonda.

Aliongeza kuwa kukmilika kwa ujenzi huo kutasaidia wakina mama 450 watkaofikishwa katika hospitali  hizo.

Katika hatua nyingine, Makonda alikabidhi magodoro 100 katika Hospitali ya Amana ambayo yayatumiwa na wazazi ambao wamekuwa wakilala wawili hadi watatu katika godoro moja.

Kwa upande wake, Meneja wa ukuzaji biashara wa kampuni ya Amsons Group,Suleiman Amon, alisema ujenzi huo utakuwa na ghorofa tatu katika hospithali ya Amana, Temeke na Mwananyamala.

Alisema ujenzi wa majengo hayo utagharimu kiasi cha Sh. Milioni 4.5 na utaanza ndani ya wiki sits kuanzia sasa na utachukua wiki nane hadi kukamilika kwake.

" Msaada huu ni kama kurudisha shukrani kwa jamii hivyo tutaendelea kuahirikiana na kuhakikisha kwamba akina mama wanapata huduma bora wakati na baada ya kujifungua,"alisema Amon.

Naye Mganga Mkuu Mkoa wa Dar es Salaam, Grace Magembe, alisema wanashukuru kwa msaada huo ambao umetolewa kwasababu utasaidia kupunguza mzigo wa changamoto waliyokuwa nayo  kwani hata watu wa mikoa ya jirani wanatumia hopspitali ya Amana kupata huduma.

"Tutatoa ushirikiano kutunza majengo hayo ili yaweze kudumu kwa muda mrefu, na magodoro yaliyoyolewa yatapunguza changamoto kwa wazazi ambao wamekuwa  wakilala watatu hadi wanne katika godoro moja,” alisema.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...