Na Emanuel Madafa, Mbeya
Katika hali isiyokuwa ya kawaida kijana  mwenye tatizo la ulemavu wa viungo na akili, amegundulika kufungiwa ndani  kwa zaidi ya miaka 11 na wazazi wake katika eneo la Mwambenja Kata ya Ilemi Jijini hapa.                                                                  
Kijana huyo, mwenye umri wa miaka 20, ambaye amejulikana kwa jina la Fredrick Emmanuel ametajwa kuwa amekuwa akiishi ndani bila ya kutolewa nje  hali iliyochangia kwa kiasi kikubwa kudhohofisha mwili wake .
Kijana Emanuel Fedrick (20) Mkazi wa Mwambenja Kata ya Ilemi jijini Mbeya   mwenye tatizo la ulemavu wa viungo na akili akiwa anaedaiwa kuwa amelala ndani kwa zaidi ya miaka 11 sasa kwa kile kinacho elezwa kuwa ni kufichwa ndani na wazazi wake ili kuondoa aibu ya familia .

Mahali anapolala  kijana Emanuel Fedrick (20)Mkazi wa Mwambeja Kata ya Ilemi jijini kwa zaidi ya Miaka 11 sasa kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kuficha aibu ya familia.

Kijana Emanuel Fedrick (20)  mwenye tatizo la utindio wa ubongo akiwa amebebwa na shangazi yake Stella Mbuligwe baada ya kutoka nje na  kufanyiwa usafi wa mwili.

Kijana Emanuel Fedrick (20) Mkazi wa Mwambenja Ilemi jijini Mbeya ambaye anatatizo la akili na ulemavu wa viungo akipelekwa ndani na shangazi yake ,Stella Mbuligwe baada ya kufanyiwa usafi na kupatiwa chakula. Picha na Emmanuel Madafa


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 21, 2016

    Mpendwa mhabarishaji wa habari HII, Kwanza napenda kutoa pongezi kwa majukumu yako ya kuhakikisha kwamba umma unapata habari mbali mbali ili kila mtu aweze kuchukua nafasi yake na kuifanya jamii yetu iwe mahali bora pa kuishi! Pili napenda kujitambulisha kwamba mimi ni miongoni mwa watu wanaoifahamu familia hiyo kwa takribani miaka minne sasa. Kwa hiyo napenda kutoa masikitiko yangu kwa mhabarishaji, kwamba taarifa hizi zimepotoshwa. Ninasema hivyo kwa sababu mimi nimemfahamu mtoto huyo kwa sababu amekuwa akitolewa nje na pia akishiriki chakula pamoja na wanafamilia wengine. Mimi mwenyewe ni shahidi, kwani nimewaona wazazi wake na wadogo zake wakimlisha. Si hivyo tu, bali wamekuwa wakimpeleka hospitali kwa matibabu; mimi mwenyewe nimeshawahi kufika katika hospitali ya Rufaa hapa Mbeya kumjulia hali mtoto huyu akiwa amelazwa. Kwa hiyo, tukio hili namna lilivyoripotiwa limeacha majeraha makubwa kwa wazazi na hata kwa mtoto mwenyewe. Napenda kutoa rai kwa wahabarishaji kufanya uchunguzi wa kina na kupata vyanzo sahihi, ili taarifa ziwe zenye kujenga badala ya kubomoa. Sio nia yangu kuanzisha malumbano katika hili, bali ninawaomba wahusika mfanye utafiti kabla ya kutoa habari. Waandishi ni kioo cha jamii, fanyeni hima kutupatia habari sahihi ili tuwe na mtizamo sahihi! Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki tasinia ya habari. Mungu iponye familia iliyojeruhiwa kutokana na upotoshwaji huu. Asanteni.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...