Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
UKITAKA kujua aina mbalimbali za vibweka vya kamati za ufundi katika michezo hasa ya soka, pamoja na aina mbalimbali za ushangiliaji basi fatilia mashindano ya Ndondo ambako ndio Mahala pake. Vibweka, vituko na kila aina ya ushangiliaji utauona hapo, Wapo wanaojipaka damu (za kuku), masizi ya mkaa, kujichora mwili mzima na hata wale wanaovaa tofauti na wengine. 

Raha ya Ndondo ni uipeleke kwenye viwanja ambavyo mashabiki wataweza kuonesha aina zao za ushangiliaji na hutataka kuamini dakika 90 zinamalizika mtu hajashuhudia hata dakika moja kwani muda wote anakuwa anafanya vibweka vinavyowaacha hoi mashabiki waliokuja kushangalia mchezo huo wa soka la mtaani maarufu kama Ndondo.

Katika uwanja wa Bandari 'Wembley'  unawapa nafasi mashabiki kufanya vituko vya kila aina na kufanya mchezo huo kugeuna ni sehemu ya burudani kwa washabiki wengine wa vibweka. 

Burudani ni kokote, kawaida ya viwanja hivi maeneo ya kukaa watu ni sehemu chache sana ila ukitaka kujua mchezo wa mpira utaona wakitumia kila aina ya njia ili kuweza kuuona. Juu ya miti, juu ya magari kote kunawezekana.
Hii ndiyo raha ya NDONDO.
Mtaalam wa Ufundi wa Timu ya Temeka Market akiwasili uwanjani huku akiwa na ulinzi wa nguvu.
Mtaalam wa Ufundi wa timu ya Kauzu FC
 Mtaalam akiwa tayari kwa kazi ya kuitafutia ushindi timu yake kutokea nje ya uwanja.
Jukwaa kuu. 

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...