Leo nimeamua kuchukua uamuzi wa kutoa agizo kali kabisa toka nimeteuliwa. 

Najua litazua maswali, lakini Kwa kuwa litaokoa maisha ya wanawake wajawazito wa nchi yetu (CEmOC) na wananchi wengine, nimelitoa. Nitalitetea. Nitalisimamia!


Nimeagiza maDED na maDMO wote nchini kuhakikisha wana theatres ZENYE KUFANYA KAZI IPASAVYO kwenye vituo vyote vya Afya kwenye maeneo yao. Wiki iliyopita nilitembelea Manispaa ya Ilala, kwenye vituo vya afya vitatu nilivyotembelea hakukuwa na theatre yenye kufanya kazi. 
Kwa mujibu wa sera ya afya ya Tanzania, 'kituo cha afya' kitakuwa na hadhi hiyo kama kina uwezo wa kufanya upasuaji. Vinginevyo hiyo ni zahanati. Mara nyingi watendaji hawa wamekuwa wakijificha kwenye kichaka cha 'hatuna fedha', wengine wakiomba fedha kutoka serikali kuu.
Nilimuuliza Mkurugenzi wa Ilala, unakusanya sh ngapi Kwa mwezi, akasema bilioni 6. Nikamuuliza unadhani ni sh ngapi kuwa na theatre yenye kufanya kazi? Akakosa jibu. Nikampa miezi 6 awe na theatre zenye kufanya upasuaji.
Leo nimefanya ziara yangu mikoa ya Shinyanga na Simiyu, nikitimiza mikoa 24. Huku pia nimekutana na tatizo hilo hilo nilipokuwa Kishapu, Shinyanga na Mwanhuzi, Simiyu. Hawa wa Meatu wenyewe wana kituo cha Afya Mwandoya, takriban Km 60 kutoka Hospitali ya Wilaya ya Meatu, pale Mwanhuzi. Wamekipa uwezo wa kufanya upasuaji. Wamenunua vifaa, wameajiri hadi Daktari (MD) kwa ajira ya muda kwa ajili ya kufanya kazi pale. Kituo kimefanya takriban operation 40, zote salama Kwa asilimia 100. Wamepunguza msongamano Mwanhuzi na wamepeleka huduma nyeti na za kuokoa maisha Karibu zaidi na wananchi, ukizingatia huku hakuna barabara za lami na hakuna ambulances. I was impressed.



Nikasema sababu za kuwa Halmashauri hazina pesa huku zinakusanya mamilioni ambayo wanayatumia bila ku-address matatizo ya msingi ya wananchi hazikubaliki. Leo iwe mwisho. Nimeagiza wakurugenzi wa Halmashauri zote nchini washirikiane na maDMO wajue watakavyofanya wahakikishe wanafungua huduma za upasuaji kwenye vituo vyote vya afya nchini ndani ya miezi sita (6).

Baada ya miezi hiyo sita mimi mwenyewe na timu yangu ya kurugenzi ya ukaguzi na uhakiki ubora wa huduma za afya (inspectorate and quality assurance) tutasambaa nchi nzima kukagua huduma hizi na pale ambapo hatutozikuta tutakishusha hadhi kituo hicho kutoka ngazi ya 'kituo cha afya' na kuwa ngazi ya 'zahanati' sambamba na kuwashauri wenzetu wa Ofisi ya Rais, TAMISEMI kuwa wakuu hao wa idara wameshindwa kutekeleza majukumu yao na hivyo wawashushe vyeo.

Nitasimamia uamuzi huu Kwa nguvu zangu zote. Sababu ni kwamba ninajua faida yake. Ninajua Mungu atafurahi, atanibariki.



Wakati wa Bunge la bajeti wanaharakati wa haki za wanawake na Watoto waliwahamasisha Wabunge watushughulikie Kwa ajili ya suala hili. Wakawa-pump wabunge data kuwa kwa siku magnitude ya vifo vinavyotokana na sababu za uzazi ni sawa na 'coaster' moja ipate ajali na iue watu wote! Wabunge waligeuka mbogo. Japokuwa namba hizi zilikuwa exaggerated (zilizidishwa), walifikisha point kwetu. Kwamba lazima tufanye kitu tofauti kwenye eneo hili. Mimi naanza kuchukua hatua. Vifo vitokanavyo na uzazi havikubaliki!



Dkt. Hamisi Kigwangalla, MB., NW-AMJW.
August 18th, 2016.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. HONGERA SANA KWA KAZI NZURI NAIBU WAZIRI MHESHIMIWA KIGWANGWALA . KAZI YAKO TUNAIONA. KEEP IT UP

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...