Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Dr. Leonard Masale (katikati) akimkabidhi kombe la ubingwa nahodha wa Barass Sports Centre baada ya timu hiyo kutwaa ubingwa wa Airtel Rising Stars mkoa wa Mwanza juzi. Kushoto ni Meneja wa Airtel Kanda ya Ziwa Ezekiel Nengwa.
Wachezaji wa Barass Sports Centre kabla ya mchezo wa fainali dhidi ya Hamas ambapo walishinda 6-1 na kutwaa uchampioni wa Airtel Rising Stars mkoani Mwanza.

TIMU ya wavulana ya Barass Sports Center imetawazwa kuwa bingwa wa mashindano ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Airtel Rising Stars mkoa wa Mwanza baada ya kuiadhibu Hamas Sports Center 6-1 katika mechi ya fainali iliyofanyika kwenye uwanja wa DIT nje kidogo ya jiji la Mwanza.
Mechi hiyo ilitanguliwa na mchezo wa kutafuta mshindi wa tatu uliozikutanisha timu za Nyamagana United na HHT ambapo Nyamagana waliibuka na ushindi mwembamba wa 1-0. Goli hilo pekee lilifungwa na Khalifan Kamanga katika dakika ya 50.

Katika mchezo wa fainali, Hamas Sports Center ndiyo waliokuwa wa kwanza kupata goli katika dakika ya 10 lililowekwa kimiani na Rogose Albert kwa shuti kali lililomshinda mlinda mlango wa Barass Sports Center.

Kuona hivyo Barass walikuja juu na kulisakama lango la wapinzani wao kama nyuki na kufanikiwa kupata goli la kusawazisha katika dakika ya 13 kupitia kwa Celuha Nehemia aliyefanya kazi ya ziada kupangua ngome ya Hamas kabla ya kuweka mpira wavuni.

Hamas walifanya mashambuli ya nguvu kwa nia ya kupata goli linguine lakini juhudi zao hakuzaa matunda na kujikuta wakifungwa goli la pili. Goli hili lilifunfuwa na mshambuliaji machachari Frank Osoro katika dakika ya 27.

Alikuwa ni Osoro tena aliyewainua mashabiki wa Barass Center baada ya kuwatoka walinzi wa Hamas na kufunga goli la tatu zikiwa zimebakia dakika mbili tu kabla ya kumaliza kipindi cha kwanza.

Barass walikianza kipindi cha pili kwa kasi na kufanikiwa kupata goli la nne katika dakika ya 55 kupitia kwa Maseke Mabigi ambaye alishirikiana vizuri na washambuliaji wenzake na kuachia shuti iliyojaa wavuni hivyo kuwakatisha tamaa wapinzani wao.
Mabigi ambaye alikuwa mwiba mkali kwa walinzi wa Hamas alifanikiwa kufunga goli la tano katika dakika ya 63 kabla ya Deo Martine kuhitimisha karamu hiyo ya magoli kwa kufunga goli la sita mnamo dakika ya 77.

Mechi za mashindano hiyo zimewawezesha makocha kuchangua kombaini ya wavulana ambayo itawakilisha mkoa wa Mwanza katika fainali za Airtel Rising Stars ngazi ya taifa zinazotarajiwa kufanyika kwenye uwanja wa kumbukumbu ya Karume jijini Dar es Salaam kuanzia September 6 hadi 11.

Timu zitakazoshiriki fainali hizo zitatoka Ilala, Kinondoni, Temeke, Zanzibar, Morogoro, Mbeya, Lindi, Mwanza na Arusha.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...