Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla ametoa maagizo mazito kwa watendaji wa Wizara hiyo kesho tarehe 22 Agosti.2016 kuhakikisha wanamfikishia taarifa ya kina kuhusu upungufu wa chanjo nchini.
Akiwa ziara ya kikazi Mkoani Geita, Ameagiza akute maelezo ya kina mezani kwake, kuwa ni nani haswa amesababisha chanjo kupungua kwenye maeneo mengi nchini? Na mpaka sasa amechukuwa hatua gani za kuwajibika?
Je, changamoto ipo hazina ama kwenye ofisi ya Mkurugenzi wa Huduma za kinga? “Vyovyote vile, nataka utetezi uje ukiwa na vielelezo, kabla sijachukua hatua stahiki. Chanjo ni eneo pekee kwenye sekta ya Afya tulilofanikiwa kwa zaidi ya 95%! Haikubaliki kurudisha nyuma mafanikio haya."
Alisema, Baadhi ya maeneo chanjo zipo na wana dozi za mwisho na baadhi hazipo kabisa. Mfano bohari ya chanjo Mkoa wa Geita hakuna chanjo za OPV, Rotavirus, BCG na Tetanus. Wangepaswa kuwa na akiba ya miezi mitatu mbele. Kwenye ngazi ya Taifa wanapaswa kuwa Na chanjo za miezi Sita mbele, hapo ndipo tunaweza kusema tuna chanjo za kutosha.
DSC_6828Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla akitoa maagizo kwa Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita, Dk. Brayan Mawalla na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Geita Dk. Joseph Kisala.
DSC_6843
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla akikagua sehemu ya dawa kwenye duka la Hospitali hiyo ya Mkoa wa Geita
DSC_6845
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Geita Dk. Joseph Kisala akitoa maelezo kwa Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla katika ziara hiyo
DSC_6899
Baadhi ya wafanyakazi wa Hospitali ya Mkoa wa Geita wakimsikiliza Naibu Waziri wa Afya Dk. Kigwangalla. Kwa picha zaidi BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...