August 9 ya kila mwaka, dunia huadhimisha Siku ya Usomaji Vitabu Kwa kila rika (International Book Lovers Day). Katika kusheherekea siku hiyo hapa nchini, Taasisi ya Doris Mollel chini ya Mwanzilishi wake, Bi. Dorice Mollel ilipata wasaa wa kutoa vitabu kwa shule tatu za jijini Dar es Salaam ambazo ni Shule za Sekondari za Tegeta na Mtakuja, pamoja na shule ya msingi ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Vitabu hivyo vilitolewa kwa ufadhili wa Rehema Trust Foundation kwenda kwa Doris Mollel Foundation.

Tegeta Sekondari ilipata vitabu ishirini na mbili (22), Mtakuja Sekondari ilipata vitabu kumi na tisa (19) na shule ya msingi ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ilipatiwa vitabu nane (8),  pamoja na kuwashirikisha wanafunzi hao kati michezo iliyotolewa kwa ufadhili wa Turkish Airways ili kusaidia watoto wapende michezo na kuchangamsha ufahamu wao.
Mwakilishi wa Taasisi ya Doris Mollel, Edward Allan akizungumza na wanafunzi wa shule ya Sekondari Tegeta kuhusu umuhimu ya kusoma vitabu vya kiada, mara baada ya kukabidhi vitabu hivyo.
Mwakilishi wa Taasisi ya Doris Mollel, Edward Allan akiwaonyesha kitu wanafunzi wa shule ya Sekondari Tegeta kwenye moja ya vitabu vilivyotolewa kwao.
Mwakilishi wa Taasisi ya Doris Mollel, Jerome Calvin (kulia) akimkabidhi vitabu Mmoja wa Wanafunzi wa shule ya Sekondari ya Mtakuja.
Wanafunzi wa Shule ya Msingi Mwalimu J.k Nyerere wakicheza na kufurahia mchezo wa chase uliotolewa na Taasisi ya Doris Mollel.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...