MKURUGENZI wa Kampuni ya Global Education Link (GEL) abdulmalik mollel amesema wanafunzi wanaokwenda vyuo vya nje ya nchi ni 350 kwa masomo ya utabibu, uhandisi, pamoja na biashara.

Akizungumza na wazazi na wanafunzi jana katika ukumbi wa mwalimu nyerere jijini dar es salaam, juu safari hiyo ,Mollel amesema kila kitu kifanyike kwa utaratibu ili kuondoa usumbufu wakati safari hiyo kwa wanafunzi hao.

Amesema wanafunzi hao wanakwenda huku tume ya vyuo vikuu nchini (TCU), ikiwa inatambua vyuo hivyo na kuwataka wazazi kuondoa hofu juu ya vyuo wanavyokwenda kusoma.

Aidha amesema Global Education Link (GEL), iko tayari kuhakikisha nchi inapata vijana wanapata elimu bora katika vyuo vya nje.

Amesema kuwa kusoma nje sio anasa kutokana na mahitaji yaliyopo vijana wanatakiwa kupata utaalam tofauti tofauti ili kuweza kufikia uchumi wa kati was viwanda.
Sehemu ya wazazi na wanafunzi na wazazi wakimsikiliza Mkurugenzi wa Global Education Link (GEL), Abdulmalik Mollel hayupo pichani katika mkutano uliofanyika jijini Dar es Salaam.


Sehemu ya wafanyakazi Global Education Link (GEL), wakiwa katika mkutano huo uliofanyika jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi wa Global Education Link (GEL), Abdulmalik Mollel akizungumza na wazazi pamoja na wanafunzi juu ya safari wanafunzi wanaokwenda kusoma katika vyuo vya nje ya nchi katika mkutano uliyofanyika jijini Dar es salaam.
Mbunge wa Mfindi Kusini, Meadrad Kigola akichangia katika mkutano huo uliofanyika jijini Dar es Salaam. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...