Kama Kristo alivyokufa na kufufuka, vivyo hivyo na hao waliolala katika Yesu, Mungu atawaleta pamoja naye I The. 4:14

Famila ya Bw. Barnaba Leo Kidulile wa Mbezi beach, Dar es Salaam tunapenda kutoa shukrani zetu za dhati kwa ndugu, jamaa, marafiki na majirani wote kwa maombi pamoja na msaada wenu wa hali na mali mliotoa katika kufanikisha mazishi ya mama yetu mpendwa Anna Mary Kidulile (pichani) aliyeitwa na Mungu tarehe 28/02/2016 katika Hospitali ya Muhimbili na kuzikwa tarehe 02/3/2016 makaburi ya Ununio Tegeta – Dar es salaam. 
Tunapenda kutoa shukrani za pekee kwa Familia ya Bw. E.P Mkwawa, Familia ya Bw. S. Ezekiel, Familia ya Bw. J. Mapunda, Familia ya Bw. B. Kimwaga na Familia ya Bw. F. Kayombo, Wana Ludewa, Mufindi, Nyanyembe na Malangali. Pia tunapenda kutoa shukrani kwa Ukoo wa kina Kilatu na Mlyuka, wafanyakazi wa TANESCO, Dar es Salaam Community BANK PLC, PPRA, TRA, Shule ya Msingi Kunduchi, waalimu na wanafunzi wa Shule ya Msingi Muhimbili na majirani wote wa Kilongawima.
Shukrani za pekee ziwaendeee mapadre wa Kanisa la Anglikana la Mtakatifu Mikael Kunduchi, wana jumuiya ya Mtakatifu Andrea, madaktari na wauguzi wa hospitali za Regency na Muhimbili. 
Kipekee tunapenda kuwaalika ndugu, jamaa na marafiki pamoja na waumini wote katika ibada ya shukrani itakayofanyika katika Kanisa la Anglikana la Mtakatifu Mikael Kunduchi, Dare es Salaam, siku ya Jumamosi ya tarehe 27 Agosti 2016 saa 3.00 kamili asubuhi na baadae chakula cha mchana. 

Ibada hiyo itatanguliwa na mkesha na maombi yatakayofanyika nyumbani kwa Familia ya Barnaba Leo Kidulile Mbezi beach - Mtaa wa Jangwani siku ya Ijumaa tarehe 26 Agosti kuanzia saa 3.00 usiku. Wote Mnakaribishwa.

Heri wenye moyo safi maana 
hao watamuona Mungu – Mt. 5:8


  

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...