Na Mary Gwera.

Mahakama ya Tanzania ‘Ardhi ni mali, ardhi ni uhai, ardhi ni uchumi,’ haya ni maneno yaliyosemwa na Mhe. Gad Mjemmas aliyekuwa Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu, Divisheni ya Ardhi. Hii ni kutokana na ukweli kuwa migogoro ya ardhi inazidi kushika kasi kila kukicha.

Aliongeza kuwa kutokana na umuhimu wa ardhi kwa maana ya kuwa na madini ndani yake, matumizi ya barabara, nyumba na miundombinu mingine kumekuwa na uhitaji mkubwa wa ardhi kwa ajili ya matumizi mbalimbali kama kilimo, ujenzi na kadhalika.

Mhe. Jaji Mjemmas anaendelea kufafanua kuwa kufuatia migogoro ya ardhi iliyokuwa ikiongezeka kila kukicha, Serikali iliona kuna haja/umuhimu wa kuundwa Tume ya Shivji iliyokuwa ikitambulika kama ‘Presidential Commission of Inquiry into Land Matters’ lengo la Tume hii ilikuwa ni kuja na mikakati ya jinsi gani ya kutatua migogoro ya ardhi.
Mhe. Jaji Gad Mjemmas, aliyekuwa Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu- Divisheni ya Ardhi (katikati), Mhe. Frank Mahimbali, Naibu Msajili, Mahakama Kuu, Divisheni ya Ardhi (kushoto) na Bw. Leonard Magacha, Mtendaji, Mahakama Kuu, Divisheni ya Ardhi wakiwa katika kikao pamoja na wadau wa Mahakama, lengo likiwa ni kupata maoni ya pamoja ya kuboresha huduma, katika kikao hicho walikubaliana kushirikiana kwa kufanya kazi kwa pamoja kuondoa kero mbalimbali.

Pamoja na mikakati mingi waliyokuja nayo, Tume hii pia ilipendekeza ianzishwe Divisheni maalum ya Mahakama kwa ajili ya kushughulikia mashauri ya ardhi, yaanzishwe pia Mabaraza ya Ardhi ya Wilaya pamoja na vijiji hii yote ililenga katika kutatua migogoro ya ardhi.

Hata hivyo; Mhe. Jaji Mjemmas aliongeza kuwa kufuatia ongezeko la mashauri na changamoto mbalimbali, Mhe. Jaji Mkuu alitoa waraka wa kuruhusu kesi za ardhi kusikilizwa na Jaji yeyote wa Mahakama Kuu ili kuweza kupunguza msongamano wa mashauri.
Mmoja wa wadau wa Mahakama (Mawakili) akieleza jambo katika kikao maalum kati ya Mahakama ya Ardhi pamoja na wadau wake (Mawakili, wadaawa n.k), kikao hicho kililenga katika kuainisha changamoto zilizopo katika usikilizaji wa Mashauri ya ardhi na mikakati ya kuzitatua ili kuondokana na mlundikano wa mashauri ya ardhi.

Jaji Mfawidhi huyo, aliainisha mikakati mbalimbali ambayo Mahakama ya Ardhi imejiwekea katika kuondoa mlundikano wa mashauri katika Mahakama hiyo.

”Mpaka kufikia mwaka jana 2015, divisheni hii ya ardhi ilikuwa na mashauri yenye umri kati ya miaka mitano (5) hadi kumi (10) 526, hivyo katika hili sisi Majaji 9 wa Mahakama ya ardhi pamoja na Wasajili tulijiwekea mikakati thabiti ya kufikia lengo la kumaliza mlundikano huu,” alisema Jaji Mjemmas.

Kuainisha matatizo ya kesi hizo: Katika hili Mhe. Mjemmas, alisema waliainisha matatizo ya kesi  hizo kwa kuchambua jalada kwa jalada ili kujua nini tatizo la kila kesi, pia walifanya uhakiki wa majalada (stock taking) kujua jala husika lipo kwa nani na kuwashirikisha Mawakili kujitoa ili kuweza kufanikisha  zoezi la kumaliza mashauri hayo.
Mjumbe akitoa maoni yake katika kikao hicho cha wadau.

Kuandaa vikao maalum ‘special session’; “ili kuweza kujikita katika kushughulikia mashauri haya, tuliandaa vikao maalum kuanzia Machi 16, 2015 hadi Aprili 30, 2015 lengo ili kufikia malengo tuliyojiwekea ya kumaliza mlundikano wa mashauri,” alifafanua, Jaji Mjemmas. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...