MBUNGE wa Rufiji Mohamed Mchengerwa ameiomba serikali kuiangalia kwa jicho la pekee wilaya ya Rufiji kwani katika mkoa wa Pwani ndiyo ambayo haina kiwanda chochote hivyo kuna umasikini mkubwa.

 Pia ameiomba kufufua kiwanda cha pamba na kusukuma Wakala wa Bonde la Mto Rufuji (Rubada) kutekeleza majukumu yake ili kuondokana na umaskini uliopo kwenye wilaya hiyo. Alisema ni zaidi ya miaka 41 sasa Rubada imekuwa haifanyi kazi yake ipasavyo na kwamba wakati wakala huo unaanzishwa kulikuwa na kiwanda cha pamba ambacho sasa kimekufa.

Kauli hiyo aliitoa  jana katika kijiji cha mkongo wakati wa uzinduzi wa Programu ya mafunzo ya kilimo na ujasiriamali kwa vijana ambayo yamefadhiliwa na Shirika la Chakula duniani(FAO) na kufunguliwa na Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Evarist Ndikilo.

 "Wilaya hii ina umasikini mkubwa tunaomba serikali ituangalie jitihada hizi za rubada leo ndizo zilitakiwa kufanyika miaka 41 iliyopita,malalamiko mengi ya wananchi yalikuwa juu yarubada itusaidie kupima ardhi.

 Tupate viwanda wilaya zote za mkoa huu hatuna kiwanda hata kimoja lakini wakati wanapewa miaka ya 70 kulikuwa na kiwanda cha pamba ila kilikuwa kimekufa na hadi sasa hakuna kiwanda chochote hapa mkoani,"alisema Mchangelwa.

 Alisema kukosekana kwa rubada hiyo kumesababisha wananchi kukosa imani na serikali yao na kwamba hiyo inatokana na kuwa nyuma kimaendeleo hivyo inabidi suala hilo lifanyiwe kazi lengo likiwa ni kurudisha imani hiyo kwa serikali yao. Aidha, aliiomba serikali kuwapa vijana wa mkoa huo elimu ya ujasiriamali ili waweze kujiajiri wenyewe badala ya kusubiri kuajiriwa.

 Akizindua mafunzo hayo,RC Ndikilo alisema uzinduzi wa mafunzo ya kilimo katika kambi ya mkongo ya namna ya kuongeza tija ya uzalishaji chakula na biashara ya awamu ya kwanza wataanza vijana 62 kutoka rufiji na nje ya mkoa wa pwani na badae watarudi katika mashamba yao kuelimisha wengine. Alisema vijana hao watapata mafunzo kwa kipindi maalum kwa hiyo na kwamba watayatumia katika maeneo mbalimbali nchini.

 "Vijana wasiendelee kuwa wahuni changamoto za ajira zinaanza kutaftiwa ufumbuzi,wasikae tu,nimefarijika kuona changamoto zinatatuliwa,vijana wapatiwe mbegu bora baada ya mafunzo na kutafutiwa masoko,"alisema.

 Alitoa Rai kwa wakuu wote wa mikoa hiyo kuunda vikundi vya vijana na kuendelezwa katika shughuli mbalimbali na kwamba Kambi hiyo iwe endelevu kwani rais mstaafu aliweka jiwe na msingi lakini hakuna kilichoendelea.

 "Tunaomba mambo haya yawe endelevu,kambi iwe mfano wa kuigwa katika mkoa wa pwani kuna zaidi ya ekari 200 ziko hapa kwa hiyo ardhi si tatizo hivyo tukiwatoa vijana vijiweni na wakija hapa msiseme hakuna ardhi maana kambi hii ni yao hivyo iwe endelevu kwa kuwapa mafunzo vijana,"alisema.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Pamoja na kuangaliwa ili viwanda vifufuliwe Viongozi wanaotaka kuinua watu wao kiuchumi waangalie uwezekano wa kubuni miradi ya maendeleo ya sehemu zao na kuhamasisha wananchi wajiunge nayo. Watafute pia michango ya watu wanaotoka maeneo hayo walioko mijini katika miradi ya maendeleo inayoweza kuinua maisha ya wananchi kwao kama kwa kuanzisha Sacco au development association ili mikopo na mitaji ya kuendeleza miradi mbalimbali ya kuondoa umasikini ipatikane. Mchango wa walio mijini wa kushirikisha wananchi katika kubadili fikra zao ili kujikwamua pia kutasaidia.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...