Kiongozi wa Urasimishaji ndugu Swagile Msananga akitoa Mada kuhusu Ujenzi na Ukarabati wa Masjala za Ardhi katika Kijiji cha Sululu Wilaya ya Kilombero Mkoani Morogoro,Uhamasishaji huu unaendelea unafanywa pia katika Vijiji Vingine unafanywa na Wizara ya Ardhi, kupitia Programu ya Kuwezesha Umilikishaji Ardhi (LAND TENURE SUPPORT PROGRAME - LTSP),Programu hii inafanya utekelezaji wake ndani ya Miaka mitatu katika Wilaya za Malinyi, Kilombero na Ulanga, Mkoano Morogoro.
Baadhi Wananchi ambao ni Wajumbe wa Halmashauri ya Kijiji cha Sululu wakiangalia ramani ya masjala ya Ardhi, inayotakiwa kujengwa katika kijiji hicho,kupitia Programu ya kuwezesha Umilikishaji Ardhi,(LAND TENURE SUPPORT PROGRAME - LTSP), mradi ambao upo chini ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.
Mmoja wa Wajumbe wa Halmashauri ya Kijiji cha Sululu Wilayani Kilombero, akichangia Mada iliyowasilishwa na Kiongozi wa Urasimishaji ndugu Swagile Msananga, iliyokuwa ikihamasisha Ujenzi wa Masjala ya kijiji,ambapo pamoja na mambo mengine,itatumika kuhifadhi hatimiliki za kimila (CCROs),ambazo zitatolewa baada ya Programu ya kupima Ardhi za Vijiji katika wilaya za Mfano za Malinyi, Kilombero na Ulanga kukamilika.
Kwa picha zaidi BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...