Mwandishi wa Habari,Mary Jovian Lyimo amefariki dunia Agosti 23 baada ya kusumbuliwa na ugonjwa wa
Kansa ya Ini, kwa mujibu wa Dada wa marehemu, Liliani Jovian Lyimo amesema kuwa
marehemu enzi za uhai wake aliwahi kufanya kazi katika Shirika la Maji Safi na
Maji Taka Dar es Salaam (DAWASCO), kama Ofisa habari wa shirika hilo, pia
alifanya kazi katika Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA).
Marehemu atazikwa leo Agosti 27 saa nane katika makaburi ya Kondo Kunduchi jijini Dar es Salaam. Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi amani.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...