Aliyekuwa msanii mahiri wa Taarab, marehemu Shakila Said wakati wa uhai wake akipongezwa na Mwenyekiti mstaafu wa CCM, Rais mstaafu wa Awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete wakati wa Tamasha la wasanii la kumuaga Mhr. Kikwete baada ya kumalizika kwa Mkutano Mkuu wa chama hicho, mjini Dodoma Julai 23, mwaka huu.
Shakila akisalimiana na Katibu Mkuu wa CCM, Komredi Abdulrahman Kinana
Aliyekuwa msanii mahiri wa Taarab, marehemu Shakila Said wakati wa uhai wake akiwa kwenye hafla hiyo
(PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA
KAMANDA WA MATUKIO BLOG)
MOLA AKULAZE PEMA "SHAKILA BINT SAIDI" :
ReplyDeleteKubwa tushukuru MUNGU, na 'Fatiha' kupigia,
Ila yatia uchungu, picha kiziangalia,
Mwezi katu timu tangu, leo umetukimbia,
PEMA MOLA AKULAZE, NASI NDIO KHATAMIA.
Ghafula umetutoka, hakuna lotarajia,
Si wa homa lalamika, wala tumbo ungulia,
Lake MOLA kiandika, 'Fayakunu' latimia,
PEMA MOLA AKULAZE, NASI NDIO KHATAMIA.
Safari ilo ya kheri, YAILAHI kujalia,
Lopituka kughufiri, adhabuze kwepushia
Ya 'Munkari wa Nakiri', wepesi kukufanyia,
PEMA MOLA AKULAZE, NASI NDIO KHATAMIA.
Nuruye akuangaze, kivuliche kukutia,
Jaza njema kuongeze, 'nari' yake kwepushia,
Jannatuye akwingize, milele humo bakia,
PEMA MOLA AKULAZE, NASI SOTE NDIO NJIA.
"Kullu Nafsi Dhaiqatul Maut"
"Inna Lillahi Wainna Ilayhi Rajiun"
Amin, Inna LILLAH wa Inna ilaihi Raajiuun,
ReplyDelete