Na Beatrice Lyimo-MAELEZO

Dar es Salaam.

31/08/2016.



RAIS Dkt. John Magufuli anatarajia kuwa mgeni rasmi katika  kongamano la tatu la kitaifa la afya  litakalofanyika jijini Dar es salaam kuanzia tarehe 14-15 Novemba, mwaka huu.


Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam Rais wa Taaasisi ya Tanzania Health Summit (THS) Dkt. Omary Chillo alisema kuwa kongamano hilo litahudhuriwa na  wadau 500 wa afya kutoka ndani na nje ya Tanzania wakiwemo watoa huduma za afya, watunga sera, watafiti wa magonjwa ya afya, wachumi, na wadau wa maendeleo.


Alisema kongamano hilo litalenga kuongeza nguvu za Serikali za kuboresha afya za Watanzania kupitia kupashana habari na ujuzi, majadiliano ya changamoto na kufikia muafaka wa njia bora za utatuzi wake ili kuimarisha huduma za afya nchini.


Aidha, alisema kuwa mkutano huo utahusisha vipengele mbalimbali ikiwemo vikao vya mashauriano yatakayogusa mada mbalimbali za maendeleo ya afya, taarifa kutoka kwa wataalamu wabobezi wa afya, pamoja na kuwasilisha matokeo ya uchunguzi.


Pia aliongeza kuwa katika kongamano hilo pia kutakuwa na maonyesho ya huduma na bidhaa kutoka kwa wasambazaji wa huduma za afya ya mashirika ya umma na binafsi.


Dkt. Chilo alitoa wito kwa wadau wa afya nchini kutoka Serikalini, mashirika binafsi, mahospital, asasi zisizo za kiserikali, taasisi za kitaaluma, wasambazaji, na washirika wa maendeleo kushiriki kikamilifu katika kongamano hilo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...