Mmoja wa wanafunzi wahitimu wa darasa la saba katika Shule ya Awali na Msingi ya Genius Kings ya jijini Dar es Salaam, akimuonesha mgeni rasmi wa mahafali ya tano ya shule hiyo, Kaimu Afisa Elimu Wilaya ya Ilala Asha Mapunda (wa pili kushoto) darubini na jinsi inavyofanya kazi. Wanafunzi 65 wa shule hiyo wanatarajiwa kuihtimu elimu ya msingi mwaka huu.
Mkurigenzi Mtendaji wa Shule ya Awali na Msingi ya Genius Kings ya jijini Dar es Salaam, Machage Kisyeri akiingiza kijiti kilichowashwa moto ndani ya ‘test tube’ kuzalisha hewa ya oksijeni ikiwa ni sehemu ya maonesho ya wahitimu wa shule hiyo wakionesha jinsi ya.Kulia ni mgeni rasmi wa mahafali ya tano ya shule hiyo, Kaimu Afisa Elimu Wilaya ya Ilala Asha Mapunda, akishuhudia.
Kikundi cha kwaya cha Shule ya Awali na Msingi ya Genius Kings ya jijini Dar es Salaam, wakiimba wimbo kwenye mahafali ya tano ya wahitimu wa darasa la saba wa shule hiyo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Kikundi cha Skauti cha Shule ya Awali na Msingi ya Genius Kings ya jijini Dar es Salaam,kikionesha umahiri katika mchezo wa Karate kwenye mahafali ya tano ya wahitimu wa darasa la saba wa shule hiyo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...