Baadhi ya wazalishaji, wanunuzi na wafanyabiashara wa madini ya jasi na makaa ya mawe wakijisajili kabla ya kuanza kwa mkutano ulioongozwa na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt Medard Kalemani hivi karibuni katika Ofisi za Wizara jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt Medard Kalemani (katikati) akizungumza na wazalishaji, wanunuzi na wafanyabiashara wa madini ya jasi na makaa ya mawe hivi karibuni katika Ofisi za Wizara jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt Medard Kalemani akizungumza mbele ya waandishi wa habari, katika mkutano uliowakutanisha wazalishaji, wanunuzi na wafanyabiashara wa madini ya jasi na makaa ya mawe (hawapo pichani) hivi karibuni katika Ofisi za Wizara jijini Dar es Salaam. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Madini, Profesa James Mdoe.

Na Veronica Simba

Serikali imepiga marufuku wawekezaji nchini kuagiza makaa ya mawe na madini ya jasi kutoka nje kwa ajili ya matumizi ya viwanda badala yake imewataka wanunue madini hayo kutoka kwa wazalishaji wa ndani.

Akizungumza hivi karibuni mbele ya waandishi wa habari katika mkutano uliowajumuisha wazalishaji, wanunuzi na wafanyabiashara wa madini ya jasi na makaa ya mawe; Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt Medard Kalemani alisema hakuna sababu ya madini hayo kuagizwa kutoka nje ya nchi kwani ipo hazina ya kutosha nchini.

Katika Mkutano huo uliofanyika Makao Makuu ya Wizara ya Nishati na Madini jijini Dar es Salaam, Dkt Kalemani alibainisha kuwa kwa upande wa makaa ya mawe, hazina iliyopo nchini kwa sasa ni zaidi ya tani milioni 5. “Madini hayo hayajachimbwa na tunataka wachimbaji wadogo na wakubwa waje wayachimbe.”

BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...