Baadhi ya wazalishaji, wanunuzi na wafanyabiashara wa
madini ya jasi na makaa ya mawe wakijisajili kabla ya kuanza
kwa mkutano ulioongozwa na Naibu Waziri wa Nishati na
Madini, Dkt Medard Kalemani hivi karibuni katika Ofisi za
Wizara jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt Medard Kalemani
(katikati) akizungumza na wazalishaji, wanunuzi na
wafanyabiashara wa madini ya jasi na makaa ya mawe hivi
karibuni katika Ofisi za Wizara jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt Medard Kalemani
akizungumza mbele ya waandishi wa habari, katika mkutano
uliowakutanisha wazalishaji, wanunuzi na wafanyabiashara
wa madini ya jasi na makaa ya mawe (hawapo pichani) hivi
karibuni katika Ofisi za Wizara jijini Dar es Salaam. Kulia ni
Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Madini, Profesa James
Mdoe.
Na Veronica Simba
Serikali imepiga marufuku wawekezaji nchini kuagiza makaa
ya mawe na madini ya jasi kutoka nje kwa ajili ya matumizi ya
viwanda badala yake imewataka wanunue madini hayo
kutoka kwa wazalishaji wa ndani.
Akizungumza hivi karibuni mbele ya waandishi wa habari
katika mkutano uliowajumuisha wazalishaji, wanunuzi na
wafanyabiashara wa madini ya jasi na makaa ya mawe;
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt Medard Kalemani
alisema hakuna sababu ya madini hayo kuagizwa kutoka nje
ya nchi kwani ipo hazina ya kutosha nchini.
Katika Mkutano huo uliofanyika Makao Makuu ya Wizara ya
Nishati na Madini jijini Dar es Salaam, Dkt Kalemani
alibainisha kuwa kwa upande wa makaa ya mawe, hazina
iliyopo nchini kwa sasa ni zaidi ya tani milioni 5.
“Madini hayo hayajachimbwa na tunataka wachimbaji
wadogo na wakubwa waje wayachimbe.”
BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI
BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...