Familia
ya marehemu Mohamed Jumanne Mtaturu Mkonongo na mkewe Bi. Naiz Edriss Mavura
pamoja na familia ya Mama Amina Mtaturu, Mheshimiwa DC Miraji Jumanne Mtaturu
na Mzee Salum Chima; tunapenda kuwashukuru ndugu, jamaa na marafiki wote kwa
upendo na faraja mliyowapatia na kwa kushiriki kwenu kikamilifu katika kufanikisha
maziko ya mpendwa wetu, Ndugu Mohamed Jumanne Mtaturu Mkonongo (pichani), ambaye aliitwa
na Mungu alhamisi, 21 Julai 2016 saa 1:40 asubuhi, kwa ajali ya gari.
Familia
inapenda kuwashukuru kipekee Wakwe wa marehemu - familia ya Mzee Edriss
Mavura; Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria,
Prof Elifas T. Bisanda pamoja na uongozi wa chuo na wafanyakazi wote wa Chuo
Kikuu Huria cha Tanzania (OUT); Uongozi na wafanyakazi wote wa Shirika la Afya
duniani (WHO) Uganda na Tanzania; Dr Harvinder Palaha wa Aga Khan Hospital, na
madaktari wenzie, wauguzi na wafanyakazi wote wa Aga Khan Hospitali kitengo cha
wagonjwa mahututi (ICU); Mzee wetu Rais
Mstaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi na familia yake; Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa
Singida, Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Ikungi; Ubalozi wa Uturuki nchini Tanzania
na Bw. Ziya Kaharan, Balozi wa Heshima wa Tanzania nchini Uturuki; Prof.
Fatmahan Atalar, Mkurugenzi wa MUHAS Genetic Laboratory ya Chuo Kikuu cha
Muhimbili; Wanajumuiya wa Ikungi Development Association (IDEA); Umoja wa
Wanafunzi waliosoma Uturuki, Masheikh wa Dar es Salaam na Ikungi; na Majirani
wote wa Dar es Salaam na Singida.
Kwa
kuwa si rahisi kumshukuru mtu mmoja mmoja, tunaomba wote mlioguswa na msiba huu
mpokee shukrani zetu za dhati.
Tunapenda
kuwataarifu kuwa Dua ya arobaini (40) ya marehemu itasomwa Jumamosi, tarehe 03
Septemba 2016, Makiungu-Ikungi, Singida, saa 5 asubuhi Wote mnakaribishwa.
INNA
LILLAHI WA INNA ILLAHI RAJIUUN
Naiz na familia poleni sana jamani kweli udongo unakula, Mungu awafariji sana
ReplyDelete