KUMBUKUMBU, mama Vailet Baraka anakumbukwa kwa mchango wake mkubwa kwa jamii hasa kuendeleza kinamama na vijana sehemu mbalimbali alipofanya kazi.

Alikuwa ni Mbunge wa kwanza kuchaguliwa na wananchi katika jimbo la Njombe Kusini 1965 mpaka 1970.(jimbo liligawanywa sasa hivi ni Ludewa) aliweza kupigania mambo mengi jimboni kuleta meli tatu jimboni, mbili zinafanya kazi mpaka kipindi hiki baada ya moja kuzama.

alitengeneza barabara  na kuanza ujenzi wa uwanja wa ndege uliopo Kijiji cha Masasi,alikuwa mchapa kazi hodari kuchelewa kazini ilikuwa mwiko.

Aalipostaafu kazi serikalini alijiajiri kwa kilimo na kufundisha hisabati na kingereza, Mama Vailet alifariki 8/6/2016. Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi.
Amina. 

si rahisi kushukuru mtu mmoja mmoja ila tunawashukuru sana sana wote mlioshiriki kwa njia moja au nyingine katika msiba huu Mungu awabariki, Tunashukuru Dr. wa hospitali ya Masiku aliemhudumia 7/6/2016, Tunashukuru Madakitari, wauguzi na wafanyakazi wa Hospitali ya Muhimbili kitengo cha mapokezi na dharula waliomhudumia 8/6/2016. 

Tunawashukuru wachungaji, uongozi na wanakwaya wa Anglican Viwege, Wa Injilisti Lutheran UDSM, Mchungaji G. Mwakyoma, familia ya marehem mzee Edward Salama, familia ya Dr. Wilson Marandu toka Arusha, familia ya Mwambona, familia ya Zacharia Namalimbogwa, familia ya  Msilu na Chale, familia ya mzee Sanga wa Namanga, familia ya Dr Mwaipopo na Sarah Botswana na Dar es Salaam, mama Mbwiga (Dar) familia ya Urassa Botswana na Dar, familia ya marehemu Dr. G.Komba wa Makongo, Pia , Asafu Haule, Mzee Timbuka, J. Chale, Shukurani sana sana David Marama(Australia), Jean Marama(U.S.A), Peter na Andrew Marama(Malawi),.

 Aidha familia inamshukuru sana Mhe. mama Anne Makinda,(Spika mstaafu) Mhe.William Lukuvi,(Waziri wa Ardhi) Mhe. Kate Kamba(Mbunge mstaafu) tunawashukuru pia kwa kusafiri toka Ludewa kuungana nasi Mhe. Deo Ngalawa Mbunge wa Ludewa, na Mhe. Stanley Kolimba.

Tunawashukuru tena sana sana wote mlioacha shughuli zenu muhimu na kuja kuungana nasi, marafiki na majirani Mungu awabariki. Asante.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...