Na. Aron Msigwa - ARUSHA.

Tanzania imeendelea kufanya vizuri katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Trakoma (Vikope) kufuatia kupungua kwa idadi ya wagonjwa na maeneo yaliyokuwa yakipata dawa za kutibu ugonjwa huo chini ya Kampeni ya utoaji wa dawa kwa watu wengi (Mass Drug Administration) iliyoanzishwa mwaka 1999.

Akizungumza kwa niaba ya Waziri Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwenye ufunguzi wa Mkutano wa pili wa mwaka wa nchi 7 za Afrika Mashariki zilizo katika mapambano dhidi ya Trakoma unaofanyika jijini Arusha, Mkurugenzi wa Tiba kutoka Wizara hiyo Dkt. Magreth Muhando amesema Tanzania imepata mafanikio hayo kutokana na juhudi kubwa zilizofanywa na Serikali na wadau mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi.

Sasa hivi wilaya 22 tumeziacha kati ya 56 zilizokuwa zikipata dawa chini ya mpango wa kutoa dawa kwa watu wengi ulioanza mwaka 1999, hii kutokana na kupata mafanikio mazuri na tunategemea kupata mafanikio zaidi kwa kuendelea kuzipunguza zilizobaki Amesema.

Ameeleza kuwa kupungua kwa idadi ya wagonjwa Trakoma nchini Tanzania mwaka hadi mwaka kunatokana na juhudi za Serikali na wadau kupitia afua mbalimbali chini mpango ujulikanao kama SAFE unaohusisha huduma za Upasuaji, utoaji wa dawa za Antibayotiki mapema, kampeni ya kuhamasisha wananchi kuosha uso pamoja na uzingatiaji wa usafi wa mazingira.

Dkt. Muhando amebainisha kuwa Trakoma umekuwa chanzo cha upofu na umasikini pale mgonjwa anapochelewa kutibiwa mapema na kusisitiza kuwa lengo la nchi hizo kukutana nchini Tanzania ni kuweka mkakati wa pamoja wa ushirikiano juu ya namna bora ya kudhibiti maabukizi ya ugonjwa huo kutoka sehemu moja hadi nyingine kutokana sababu za kijiografia na mwingiliano wa watu kutoka nchi moja moja hadi nyingine hali inayoweza kuchangia kusambaza ugonjwa huo.

Amesisitiza kuwa bado watanzania wanalojukumu la kuhakikisha ugonjwa huo unatoweka katika maeneo yao kwa kuzingatia na kufuata kanuni za afya, kufanya usafi wa mwili hususan uso kila siku kwa maji safi na sabuni pamoja na kufanya usafi wa mazingira ili kudhibiti kuenea kwa ugonjwa huo.

Mkurugenzi wa Tiba kutoka Wizara hiyo Dkt. Magreth Muhando akizungumza kwa niaba ya Waziri Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwenye ufunguzi wa Mkutano wa pili wa mwaka wa nchi 7 za Afrika Mashariki zilizo katika mapambano dhidi ya Trakoma unaofanyika jijini Arusha.
Mratibu wa Taifa wa Magonjwa yasiyopewa kipaumbele kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Upendo John Mwingira akizungumza wakati wa mkutano wa pili wa mwaka wa nchi 7 za Afrika Mashariki zilizo katika mapambano dhidi ya Trakoma unaofanyika jijini Arusha.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Kimataifa ya kupambana na Trakoma (International Trachoma Initiative) Dkt. Paul Emerson akizungumza katika Mkutano huo ambapo ameipongeza Tanzania kwa kazi nzuri inayofanya ya kuhakikisha ugonjwa wa Trakoma unatokomezwa.

Washiriki wa mkutano huo kutoka nchi 7 za Bara la Afrika wakiwa katika picha ya pamoja.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...