Na. Aron Msigwa - ARUSHA.
Tanzania
imeendelea kufanya vizuri katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Trakoma
(Vikope) kufuatia kupungua kwa idadi ya wagonjwa na maeneo yaliyokuwa
yakipata dawa za kutibu ugonjwa huo chini ya Kampeni ya utoaji wa dawa
kwa watu wengi (Mass Drug Administration) iliyoanzishwa mwaka 1999.
Akizungumza
kwa niaba ya Waziri Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
kwenye ufunguzi wa Mkutano wa pili wa mwaka wa nchi 7 za Afrika
Mashariki zilizo katika mapambano dhidi ya Trakoma unaofanyika jijini
Arusha, Mkurugenzi wa Tiba kutoka Wizara hiyo Dkt. Magreth Muhando
amesema Tanzania imepata mafanikio hayo kutokana na juhudi kubwa
zilizofanywa na Serikali na wadau mbalimbali kutoka ndani na nje ya
nchi.
Sasa hivi wilaya 22 tumeziacha kati ya 56 zilizokuwa
zikipata dawa chini ya mpango wa kutoa dawa kwa watu wengi ulioanza
mwaka 1999, hii kutokana na kupata mafanikio mazuri na tunategemea
kupata mafanikio zaidi kwa kuendelea kuzipunguza zilizobaki Amesema.
Ameeleza
kuwa kupungua kwa idadi ya wagonjwa Trakoma nchini Tanzania mwaka hadi
mwaka kunatokana na juhudi za Serikali na wadau kupitia afua mbalimbali
chini mpango ujulikanao kama SAFE unaohusisha huduma za Upasuaji,
utoaji wa dawa za Antibayotiki mapema, kampeni ya kuhamasisha wananchi
kuosha uso pamoja na uzingatiaji wa usafi wa mazingira.
Dkt.
Muhando amebainisha kuwa Trakoma umekuwa chanzo cha upofu na umasikini
pale mgonjwa anapochelewa kutibiwa mapema na kusisitiza kuwa lengo la
nchi hizo kukutana nchini Tanzania ni kuweka mkakati wa pamoja wa
ushirikiano juu ya namna bora ya kudhibiti maabukizi ya ugonjwa huo
kutoka sehemu moja hadi nyingine kutokana sababu za kijiografia na
mwingiliano wa watu kutoka nchi moja moja hadi nyingine hali inayoweza
kuchangia kusambaza ugonjwa huo.
Amesisitiza kuwa bado watanzania
wanalojukumu la kuhakikisha ugonjwa huo unatoweka katika maeneo yao kwa
kuzingatia na kufuata kanuni za afya, kufanya usafi wa mwili hususan
uso kila siku kwa maji safi na sabuni pamoja na kufanya usafi wa
mazingira ili kudhibiti kuenea kwa ugonjwa huo.
Mkurugenzi wa Tiba kutoka Wizara hiyo Dkt. Magreth Muhando akizungumza kwa niaba ya Waziri Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwenye ufunguzi wa Mkutano wa pili wa mwaka wa nchi 7 za Afrika Mashariki zilizo katika mapambano dhidi ya Trakoma unaofanyika jijini Arusha.
Mratibu wa Taifa wa Magonjwa yasiyopewa kipaumbele kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Upendo John Mwingira akizungumza wakati wa mkutano wa pili wa mwaka wa nchi 7 za Afrika Mashariki zilizo katika mapambano dhidi ya Trakoma unaofanyika jijini Arusha.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Kimataifa ya kupambana na Trakoma (International Trachoma Initiative) Dkt. Paul Emerson akizungumza katika Mkutano huo ambapo ameipongeza Tanzania kwa kazi nzuri inayofanya ya kuhakikisha ugonjwa wa Trakoma unatokomezwa.
Na. Aron Msigwa - ARUSHA.
Tanzania imeendelea kufanya vizuri katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Trakoma (Vikope) kufuatia kupungua kwa idadi ya wagonjwa na maeneo yaliyokuwa yakipata dawa za kutibu ugonjwa huo chini ya Kampeni ya utoaji wa dawa kwa watu wengi (Mass Drug Administration) iliyoanzishwa mwaka 1999.
Akizungumza kwa niaba ya Waziri Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwenye ufunguzi wa Mkutano wa pili wa mwaka wa nchi 7 za Afrika Mashariki zilizo katika mapambano dhidi ya Trakoma unaofanyika jijini Arusha, Mkurugenzi wa Tiba kutoka Wizara hiyo Dkt. Magreth Muhando amesema Tanzania imepata mafanikio hayo kutokana na juhudi kubwa zilizofanywa na Serikali na wadau mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi.
Sasa hivi wilaya 22 tumeziacha kati ya 56 zilizokuwa zikipata dawa chini ya mpango wa kutoa dawa kwa watu wengi ulioanza mwaka 1999, hii kutokana na kupata mafanikio mazuri na tunategemea kupata mafanikio zaidi kwa kuendelea kuzipunguza zilizobaki Amesema.
Ameeleza kuwa kupungua kwa idadi ya wagonjwa Trakoma nchini Tanzania mwaka hadi mwaka kunatokana na juhudi za Serikali na wadau kupitia afua mbalimbali chini mpango ujulikanao kama SAFE unaohusisha huduma za Upasuaji, utoaji wa dawa za Antibayotiki mapema, kampeni ya kuhamasisha wananchi kuosha uso pamoja na uzingatiaji wa usafi wa mazingira.
Dkt. Muhando amebainisha kuwa Trakoma umekuwa chanzo cha upofu na umasikini pale mgonjwa anapochelewa kutibiwa mapema na kusisitiza kuwa lengo la nchi hizo kukutana nchini Tanzania ni kuweka mkakati wa pamoja wa ushirikiano juu ya namna bora ya kudhibiti maabukizi ya ugonjwa huo kutoka sehemu moja hadi nyingine kutokana sababu za kijiografia na mwingiliano wa watu kutoka nchi moja moja hadi nyingine hali inayoweza kuchangia kusambaza ugonjwa huo.
Amesisitiza kuwa bado watanzania wanalojukumu la kuhakikisha ugonjwa huo unatoweka katika maeneo yao kwa kuzingatia na kufuata kanuni za afya, kufanya usafi wa mwili hususan uso kila siku kwa maji safi na sabuni pamoja na kufanya usafi wa mazingira ili kudhibiti kuenea kwa ugonjwa huo.
Mkurugenzi wa Tiba kutoka Wizara hiyo Dkt. Magreth Muhando akizungumza kwa niaba ya Waziri Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwenye ufunguzi wa Mkutano wa pili wa mwaka wa nchi 7 za Afrika Mashariki zilizo katika mapambano dhidi ya Trakoma unaofanyika jijini Arusha.
Mratibu wa Taifa wa Magonjwa yasiyopewa kipaumbele kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Upendo John Mwingira akizungumza wakati wa mkutano wa pili wa mwaka wa nchi 7 za Afrika Mashariki zilizo katika mapambano dhidi ya Trakoma unaofanyika jijini Arusha.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Kimataifa ya kupambana na Trakoma (International Trachoma Initiative) Dkt. Paul Emerson akizungumza katika Mkutano huo ambapo ameipongeza Tanzania kwa kazi nzuri inayofanya ya kuhakikisha ugonjwa wa Trakoma unatokomezwa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...