NA LEAH MUSHI
Chama cha watanzania waliosoma China- CHINA ALLUMNI ASSOCIATION OF TANZANIA (CAAT) hii leo tarehe 27 August, 2016 kinatarajia kufanya uchaguzi mkuu kwa ajili ya kupata viongozi wake wapya.

Uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika katika ukumbi wa Rombo Green views Hotel sinza Dar es salaam kuanzia saa saba kamili mchana nakufuatiwa na sherehe ya kuwapongeza viongozi wapya na kuwaaga viongozi waliomaliza muda wao.

Kwa mujibu wa mwenyekiti wa uchaguzi wa chama hicho GUSTAV SANGA uchaguzi huo utawaweka madarakani viongozi hao miaka mitatu kwa mujibu wa katiba ya chama hicho.

Nafasi zinazogombewa katika uchaguzi huo ni Chairperson, Secretary, Treasurer, Director of Statistics, media and information, director of Art, culture and heritage pamoja na Director of Education, Science and Technology
SANGA pia amewakaribisha watanzania wote waliomaliza China kujiunga katika chama hicho ili kuweza kutimiza malengo mbalimbali waliyojiwekea ikiwemo kuishauri serikali masuala yahusuyo TANZANIA- CHINA.

Chama hicho cha watanzania waliosoma China kina miaka sita tangu kuanzishwa kwake na kina wanachama tangu waliosoma china miaka ya1980 kwa ngazi ya shahada , astashahada na shahada ya uzamivu. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...