Waziri wa Mambo ya Katiba na Sheria Mh. Dkt. Harrison Mwakyembe (kushoto) akisisitiza jambo kwa wageni wake Mkuu wa Kitengo cha Kupambana na Biashara haramu ya dawa za Kulevya kutoka Shirika la umoja wa mataifa la kupambana na dawa za kulevya na uhalifu (UNODC) Bw. Johan Kruger (kulia), Mratibu wa kupambana na uhalifu wa majini Bi. Kaitlin Meredith (wa pili kulia) na mwingine ni mtendaji kutoka UNODC walipomtembelea ofisini kwake leo jijini Dar Es Salaam.
Waziri wa Mambo ya Katiba na Sheria Mh. Dkt. Harrison Mwakyembe (kushoto) akimsikiliza kwa makini Mkuu wa Kitengo cha Kupambana na Biashara haramu ya dawa za Kulevya kutoka Shirika la umoja wa mataifa la kupambana na dawa za kulevya na uhalifu (UNODC). Bw. Johan Kruger (wa pili kulia) alipomtembelea ofisini kwake leo jijini Dar Es Salaam kwa ajili ya kubadilishana mawazo. Wengine pichani ni watendaji kutoka Shirika la umoja la kupambana na dawa za kulevya na uhalifu na Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Katiba kutoka Wizara ya Mambo ya Katiba na Sheria Bi. Mercy Mrutu (wa kwanza kulia).
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...