Na mwandishi wetu, Durham, NC

Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani na Mexico, Mhe. Wilson Masilingi siku ya Ijumaa Septemba 2, 2016 alimtembelea na kufanya mazungumuzo na Mayor wa mji wa Durham, North Carolina, Mayor William V. "Bill Bell".

Katika mazungumuzo hayo yaliyofanyika ofisi ya Mayor iliyopo City Hall, Mhe. Balozi Wilson Masilingi alimweleza Mayor William "Bill Bell" nia yake ya kutafuta wawekezaji watakaosaidia kukuza uchumi wa Tanzania kupitia seka mbalimbali huku akimweleza juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Magufuli za kufufua na kujenga viwanda,

Mhe. Balozi Wilson Masilingi alimhakikishia Mayor William "Bill Bell" wawekezaji watakaokua tayari kuwekeza Tanzania watafanyia taratibu zote na kwa haraka zaidi na bila kuwa na usumbufu huku Mayor William "Bill Bell" akimuahidi Mhe. Balozi William Masilingi kutoa ushirikiano wa karibu na kuhakikisha anamkutanisha na wawekezaji wa Durham, North Carolina watakaokua tayari kuwekeza nchini Tanzania.
Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani na Mexico, Mhe. Wilson Masilingi akifanya mazungumuzo na Mayor wa mji wa Durham Mayor William"Bill Bell"
Mazungumuzo yakiendelea wengine katika mazungumuzo hayo kutoka kushoto kwa mzunguko wa meza ni Afisa Uhamiaji wa Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani, Bwn. Abbas Missana, Brady Surles ambaye ni Mkurugenzi mtendaji wa Sister Cities ya Durham yenye mashirikiano na mji wa Arusha, Tony Nturu, Dorothy Borden ambaye ndie mwanzilishi wa Sister Cities na Mwenyekiti wa Umoja wa Watanzania North Carolina, Bi. Gloria Alex,
Mazungumuzo yakiendelea.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...