Shirika la Maji Safi na Majitaka Dar-es-salaam (DAWASCO), linawatangazia  wakazi wa jiji la Dar-es-salaam na  Mji wa Kibaha mkoan Pwani kuwa Mtambo wa kuzalisha Maji wa Ruvu Juu utazimwa kwa wastani wa Saa 14, kuanzia saa 3:00 asubuhi hadi saa 05:00 usiku, siku ya Ijumaa tarehe 02/09/2016.

Sababu ya kuzimwa kwa Mtambo wa Ruvu Juu ni kuruhusu usafishaji wa bomba jipya na kufanya majaribio ya sehemu ya mtambo mpya wa Maji wa Ruvu Juu, Zoezi hili linaashiria hatua za mwisho za upanuzi wa mtambo huo, ili kuondoa tatizo la upatikanaji wa huduma ya Maji katika maeneo yanayohudumiwa na mtambo wa Ruvu Juu.

Kuzimwa Kwa mtambo wa Ruvu Juu kutapelekea maeneo yafuatayo kukosa Maji:

MLANDIZI MJINI, RUVU DARAJANI, VIKURUTI, DISUNYARA, KILANGALANGA, JANGA, MBAGALA, VISIGA, MAILI 35, ZOGOWALE, MISUGUSUGU, TANITA, KIBONDENI, KWA MATHIAS, NYUMBU, MSANGANI, KWA MBONDE, PICHA YA NDEGE, SOFU, LULINZI, GOGONI, KIBAMBA, KIBAMBA NJIA PANDA SHULE KIBWEGERE, MLOGANZIRA, KWEMBE, KIBAMBA HOSPITALI, KWA MKINGA, NA LUGURUNI.
WANANCHI MNASHAURIWA KUHIFADHI MAJI NA KUYATUMIA KWA MATUMIZI YA LAZIMA

DAWASCO INAOMBA RADHI WANANCHI WA MAENEO HUSIKA KWA USUMBUFU UTAKAOJITOKEZA.

Kwa taarifa zaidi wasiliana nasi kupitia kituo cha huduma kwa wateja 022-2194800 au 0800110064 (BURE).
IMETOLEWA NA:
OFISI YA UHUSIANO
DAWASCO-MAKAO MAKUU

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...