Na Mathias Canal, Singida

Uongozi wa Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida umeahidi kuvisaidia vikundi mbalimbali ambavyo vitakubali kujihusisha na kilimo cha mbogamboga na matunda (Perishable Crops) sambamba na kilimo hicho kwa kutumia Kitalu Nyumba (Green House).

Kauli ya serikali imetolewa na Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe Miraji Jumanne Mtaturu wakati akifunga mafunzo kwa wajasiriamali, wakulima na wafugaji yaliyoendeshwa na Asasi isiyo ya kiserikali ya Right Way For Development (RIWADE) kwenye ukumbi wa Mikutano katika Shule ya Sekondari Ikungi na kuhudhuriwa na watu 115 ambao wanatokea katika Kata 24 kati ya Kata 28 zilizopo Wilayani humo.

Katika Mafunzo hayo jumla ya Vikundi 39 vimehudhuria ambavyo vimetakiwa kujishughulisha zaidi kukimbia kilimo cha mazoea ambacho wakulima hulima msimu mmoja hadi mwingine na hatimaye kujihusisha na kilimo cha umwagiliaji ambacho kinatumia muda mchache kukamilika na kuanza kwa mavuno.

DC Mtaturu amevitaka vikundi hivyo kwa pamoja kutumia vyema fursa ya Makao makuu ya serikali kuhamia Mjini Dodoma kwani itakuwa taswira chanya katika kukuza soko la mazao yao pasina kupata ugumu wa uuzaji.

Amesema kuwa Mkoa wa Singida mara nyingi umekuwa ukitajwa kama mkoa masikini nchini Tanzania kati ya mikoa 10 ambayo ipo mkiani katika maendeleo ya kiuchumi kwa sababu ya wananchi wenyewe kutofanya ubunifu katika kilimo chao jambo ambalo linasababisha uzalishaji mdogo na kupelekea kipato kuendelea kuwa duni ilihali maandalizi ya mashamba ni makubwa.

Mtaturu amesema kuwa wananchi wanapaswa kutoa ushirikiano kwa serikali katika kukamilisha adhma yake katika uwekezaji na Tanzania ya viwanda kwani endapo watakubali kulima kilimo cha kisasa na kuwa na uzalishaji mkubwa itakuwa rahisi kwa serikali kuanzisha viwanda vya kusindika mazao.

Kwa upande wake muwezeshaji wa mafunzo hayo ambaye pia ni Mkurugenzi wa Asasi isiyo ya kiserikali ya RIWADE ambayo imesajili kwa lengo la kiwasaidia vijana wasio na ajira waweze kufanya kilimo, Ufugaji, Uvuvi na Mazingira Mhandisi Ayubu Massau alisema kuwa wananchi wanapaswa kufikia kilimo cha kuachana na kuuza mazao yao kwa madalali badala yake kuuza moja kwa moja kwa mtumiaji jambo ambalo litatoa fursa chanya ya mafanikio makubwa katika pato la mwananchi mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla.

Hata hivyo amepigia chepuo zaidi kilimo cha Kitalu Nyumba (Green House) na kusema kuwa ndicho kilimo pekee chenye uwezo wa kuwatoa wananchi kwenye kadhia ya umasikini kwani kilimo hichp kupitia umwagiliaji wa kisasa unatumia maji machache na matokeo yake ni makubwa kama wakulima watafuata taratibu zote za utunzaji wa shamba.

Massau alisema kuwa umefika wakati wa wananchi kuachana na vyama vya kufa na kuzikana badala yake kujihusisha zaidi na vyama vya kujikwamua kiuchumi kupitia vikundi mbalimbali.
Kutoka Kushoto ni Mkurugenzi wa Asasi isiyo ya kiserikali ya RIWADE Mhandisi Ayubu Massau, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi, Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu, Moses Msai Mratibu wa RIWADE mkoa wa Singida na Afisa kilimo wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Ayub Sengo
Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu na kulia kwake ni Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Bi Haika Massawe wakifatiliakwa makini mafunzo ya namna bora ya kujishughulisha na kilimo cha umwagiliaji kwa kutumia Gree House
Kutoka Kushoto ni Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM Hassan Tati, Mkurugenzi wa Asasi isiyo ya kiserikali ya RIWADE Mhandisi Ayubu Massau, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Bi Haika Massawe, Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mhe Miraji Jumanne Mtaturu, Moses Msai Mratibu wa RIWADE mkoa wa Singida na Afisa kilimo wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Ayub Sengo

Dc Mtaturu akisisitiza jambo wakati wa kufunga mafunzo hayo.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...