Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga, Stephen Magoiga amekutana na watendaji wa kata na vijiji wilayani humo.

Magoiga amewataka hao kuhakikisha wanawajibika katika ukusanyaji wa mapato ya Serikali badala ya kuacha watu wanakwepa kutimiza wajibu wao.

Alisema watendaji wanapaswa kuhakikisha sheria za nchi zinafuatwa ikiwemo kulipa kodi na ushuru mbalimbali ili Serikali ipate mapato na kuweza kuwahudumia wananchi.

“Ukusanyaji mapato uwe ajenda muhimu na mtendaji ana uwezo wa kulisimamisha gari lenye mzigo wa mazazo mahali popote kwenye himaya yake na kuhakikisha limelipa kodi.

“Hakikisheni mageti yanafanya kazi ninyi ni walinzi wa amani katika kata zenu kwa hiyo sitaki kuona sheria zinakiukwa, tuache kufanya kazi kwa mazoea,” alisema.

Aidha, mkurugenzi huyo alionya tabia ya baadhi ya watendaji na watalaamu mbalimbali kushinda maofisini badala ya kuwatembelea na kuwahudumia wananchi.

Alisisitiza maofisini ni mahali pa vikao vya ndani tu na kuwa hatapenda kuona wananchi wakikosa huduma kutokana na kutofikiwa na watalaamu au watendaji.

Magoiga alitaka ushirikiano katika utendaji huku akikemea utoro katika vituo vya kazi na kwamba mtendaji anapaswa kuhakikisha watumishi wote ngazi ya kata wanakuwepo vituoni kwao.

“Utakuta mtumishi hayupo huku mtendaji kata hana taarifa yoyote hiyo ni kazi ya mazoea, kila siku nasema sitaki kazi za mazoea, tuwajibike kwa wananchi wetu,” alisisitiza.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Stephen Magoiga (wa pili kushoto) akizungumza na watendaji wa kata na vijiji katika kikao kazi kilichofanyika ukumbi wa halmashauri. Wengine pichani ni kuanzia kushoto ni Afisa Utumishi na Utawala, Jumanne Chaula, Mwanasheria wa Wilaya, Wilson Nyamunda na Afisa Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika Wilaya, George Kessy.
Mkuu wa Wilaya ya Kishapu, Nyabaganga Taraba akizungumza na watendaji katika kikao hicho.
Watendaji wa kata na vijiji wa Kishapu wakifuatilia maelekezo kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji, Stephen Magoiga wakati wa kikao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...