WANAFUNZI wataokosa nafasi za vyuo vikuu bado na wana nafasi ya kujiunga na vyuo vikuu vya nje kupitia Global Education Link (GEL).

Hayo ameyasema leo Mkurugenzi Mtendaji wa Global Education Link (GEL), Abdulmaalik Mollel wakati kuondosha wanafunzi 200 kwenda katika vyuo vikuu vya nchini China, amesema GEL ni kampuni inayoongoza kupeleka wanafunzi kwenda vyuo vikuu vya nje vya Afrika Mashariki hivyo wazazi watumie nafasi kupeleka wanafunzi katika vyuo vya nje.

Amesema kuwa Global Education Link(GEL) ina uhakika wanafunzi watakayehitimu watakuwa na mchango mkubwa kwa taifa katika Teknolojia ya uhandisi wa petrol , Biashara pamoja na utabibu.

Mollel amesema kuwa wanafunzi wanaweza kukopeshwa kwa asilimia 50 na kulipa ndani miezi sita ikiwa kuhakikisha wanafunzi wanatimiza ndoto zao n kuwa na mchango a taifa. Aidha amesema kuwa wanafunzi wanaokwenda mazingira ya usalama ni uhakika kwa kuanza kwa safari hadi wanafika katika vyuo husika .

Mollel amesema kuwa vijana wasikate tamaa Global Education Link (GEL) iko kwa ajili ya yao katika kuhakikisha ndoto zao hazipotei kutokana na kukosa nafasi katika vyuo vya ndani

Amesema kuwa wazazi waache kuogopa gharama za kusoma vyuo vya nje kwani gharama za kusoma nje ni sawa na vyuo vya ndani hivyo vijana watumie furssa hizo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Global Education Link (GEL), Abdulmaalik Mollel akizunguza waandishi wa habari leo wakati akisafirisha wanafunzi 200 kwenda vyuo vikuu vya nchini China katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
Wafatnyakazi wa Global Education Link (GEL) wakifanya uhakiki wa hati za kusafiria pamoja na Viza kwa wanafunzi wanaokwenda kusoma vyuo vikuu vya China leo katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wanafunzi wanaokwenda Vyuo Vikuu nchini China wakiagana na familia zao kwa kupiga picha ya pamoja katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere leo jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wanafunzi wanaokwenda katika Vyuo Vikuu nchini China wakiingia kwenye jengo la maalumu la ukaguzi kabla ya kuanza safari katika uwanja huo Jijini Dar es Salaam. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...