Sallam kutoka WCB ameonyesha baadhi ya nyaraka ambazo zimewapitia kibali cha kutumia sehumu za wimbo ‘Maria Salome’ wa Saida Karoli katika wimbo mpya wa Diamond, ‘Salome’.
Wimbo ‘Maria Salole’ wa Saidi Karoli ni miongoni mwa nyimbo za asili zilizofanya vizuri miaka ya 2000.Hali hiyo iliufanya uongozi wa Diamond kuzungumza na uongozi wa Saida Karoli ili upate kibali cha kutumia sehemu za nyimbo hiyo.
“Tunakushukuru sana uongozi wa Saida Karoli na mzee Felician Mutakyawa kutupa haki na baraka zote kutumia wimbo wa Maria Salome,” aliandika Sallam instagram. “Tunatambua kwamba nyimbo hii itaendelea kuwa moja ya nyimbo bora kuwahi kutoka katika nchi ya Tanzania,”
Diamond kupitia wimbo huu amerudi tena katika nyimbo za asili baada ya kufanya vizuri na wimbo ‘Mdogo Mdogo’ miaka miwili iliyopita.
Pichani juu anaonekana Diamond na Rayvanny wakiwa na Mzee Felician Mutakyawa wakati wa kusaini makubaliano ya kutumia sehemu ya wimbo huo wa 'SALOME' ambao umebamba kila kona.
CHANZO: BONGO FIVE
Hakuna mwengine zaidi ya Diamond.
ReplyDeleteAisee Naseeb, hapa ndipo anapowaacha mbali artists wengine wa Bongo kwa ubunifu wake.... Diamond hakika yupo juu, wengine watafuata nyuma tuu, watake wasitake.
ReplyDeleteEndelea na uzi huo huo!
jamaa anajua sana
ReplyDeleteMasha Allah! Kwa kweli hii 'version' ya 'Maria Salome' iliyoimbwa na Diamond Platnumz ft Rayvanny, ipo very 'classic'. Hakika mnastahili pongezi za pekee kwa kazi nzuri, kuanzia midundo (muziki) , uchezaji na hata ujumbe 'makhsusi' uliyomo katika wimbo huo, kwa kweli wenye wivu wajinyonge tu. Hakika mnastahili sifa na pongezi za pekee 'crew' nzima ya WCB kwa ushirikiano wenu.
ReplyDeleteSafi sana,, ila kama haujasoma magazeti ya leo basi SOMA HAPA
ReplyDeleteSanaa ni ubunifu, mmeutendea haki huu wimbo, mmewaacha 'kodo', hongereni sana Diamond na team nzima ya WCB
ReplyDelete