Na Beatrice Lyimo- MAELEZO, Dodoma

Serikali imesema ni kinyume cha sheria kwa askari mgambo kuwanyanyasa Mama Lishe na wafanyabiashara wengine wadogo nchini.

Akijibu swali la Mhe. Zaynab Vulu (Viti Maalumu) alilotaka kujua kwanini Serikali isiandae mazingira mazuri ya kufanyia kazi wafanyabiashara hao, Naibu Waziri Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI) Mhe. Seleman Jaffo amemesema kuwa askari mgambo wanapaswa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu bila kuwanyanyasa wala kuwadhulumu wakati wakiwaondoa katika maeneo yasiyoruhusiwa.

Naibu Waziri Jaffo aongeza kuwa Serikali inatambua na kuthamini mchango wa wafanyabiashara hao walioko katika sekta isiyo rasmi katika kukuza kipato na ajira.Aidha, Naibu Waziri Jaffo amesema kuwa Serikali haitasita kuchukua hatua kwa askari mgambo yeyote atakayebainika kujihusisha na vitendo vya kuwanyanyasa wafanyabiashara na Mama Lishe wanapotekeleza majukumu yao.

Mbali na hayo, Naibu Waziri amezikumbusha Halmashauri zote nchini kutenga maeneo kwa ajili ya wafanyabiashara ndogo ndogo wakiwemo Mama Lishe karibu na maeneo walipo wateja wao.

Zaidi ya hayo Naibu Waziri huyo amewataka wafanyabiashara wadogo nchini kufanya biashara katika maeneo yaliyotengwa rasmi na Halmashauri na kuacha kufanya biashara hizo katika maeneo yasiyoruhusiwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...